HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 3, 2019

LIVERPOOL MABINGWA WA LIGI YA MABINGWA ULAYA KWA MARA YA SITA BAADA YA KUILAZA TOTTENHAM

Liverpool ndio Mabingwa wa Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya sita baada ya kuilaza Tottenham katika mechi ilioshirikisha timu mbili za Uingereza jijini Madrid.

Mohamed Salah alifunga goli la penalti baada ya dakika mbili kufuatia  Moussa Sissoko aliyeshikishwa mpira na Sadio Mane katika eneo hatari.

Zaidi ya mashabiki 1600 wa Kitanzania, waliweza kufurahia fursa ya kipekee ya kutazama fainali hizo katika mazingira safi ambapo miamba wa soka Liverpool kutoka nchini Uingereza walikutana na wapizani wao kwa ligi ya EPL Totenham Hotspurs. Katika mtanange huo, Liverpool walitawazwa mabingwa baada ya kuwalaza  Totenhan Hotspurs kwa    mabao      2-0 .

Ikiwa mmoja wa wadhamini wakuu wa ligi hiyo maarufu na inayotizamwa na mamilioni ya watu kote duniani, Heineken iliweza kuwaleta pamoja Watanzania chini ya bia yao pendwa ya Heineken na kupata fursa ya kutazama fainali hizo.

Meneja wa Heineken Tanzania Lungisa Adams alisema,  “Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya ni moja kati ya ligi zinazohusisha wachezaji wakubwa. Timu zote bora barani Ulaya zinashiriki ligi hii. Kwa upande mwingine, bia ya Heineken ni bia inayojulikana na kutumiwa na watu wengi kote duniani  na kwa hiyo kuna uhusiano kati ya Heineken na ligi ya mabingwa. Mwaka huu, wateja wetu siyo tu hawatafurahia kutazama ligi bali pia kushiriki fursa zinazokuja na ligi,”
 Aliongeza  “Bia ya Heineken inatengeneza msisimko katika ligi hii kubwa duniani kwa kuwaleta pamoja kwa mamna ya pekee ambayo ni Heineken tu wanafanya. Kwa Tanzania, Heineken imetoa haki za kipekee kwa mashabiki kuweza kushiriki katika kutizama fainali katika mazingira tulivu na ya aina yake kwenye eneo la NEXT Door Arena.  Fainali hii pia ilitizamwa katika sehemu tofauti tofauti 8 mbali mbali nchini.”
Lungisa aliongeza kuwa, wateja wa Heineken waliweza kushiriki pamoja na kubadilishana taarifa za matukio wakati wakitazama fainali kupitia kibwagizo  #ShareUnmissableMoments
“Tunafurahi kuwa bia ya Heineken ni bia ya Watanzania na siku zote wamekuwa sehemu ya kile tunachokifanya na hata wanahamu kunywa zaidi bia zetu,” aliongeza.
 Alisema ikiwa kama bia yenye jina kubwa, siku zote imekuwa ikidhamini na kuwekeza kwenye michezo ambayo inayowagusa wateja wake na kuwaleta pamoja katika masoko yanayochipukia kama Tanzania.
Wakati wa fainali hizo, Heineken ilimleta msaniii wa bongo fleva Ray Vanny Kuwafurahisha wateja wake na pia iliwazawadia bidhaa mbali mbali zinazotokana na ligi hiyo.  
Heineken imekuwa mdau wa UEFA tangu mwaka1994
Mwaka 2005, Heineken iliichukua Heineken iliyokuwa inamilikiwa na Amstel
Heineken italeta udhamini kwa nchi zaidi ya 220 kupitia kampeni za kimasoko na mawasiliano kwa umma.
Ligi ya Mabingwa inatazamwa na zaidi ya watu bilioni 4.2 kote duniani.
Tangu mwaka 2007, kombe la UEFA linalotembezwa na Heineken, limefika zaidi ya nchi 35 ikiwamo Afrika, Asia Amerika ya Kaskazini na Kusini
Kufuatia kusainiwa kwa mkataba mpya, Heineken itaendea kuidhamini UEFA hadi kufikia msimu wa mwaka2020/2021.Mashabiki wa Liverpool wakishangilia kwa msisimko baada ya timu yao kutwaa Kombe la Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya sita, wapenzi wa kandanda zaidi ya 1,600 walijikusanya katika ukumbi wa Next Door Arena, jijini Dar es Salaam.
 Mashabiki wa Liverpool wa wameshika mfano wa kombe   baada ya timu yao kutwaa Kombe la Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya sita, wapenzi wa kandanda zaidi ya 1,600 walijikusanya katika ukumbi wa Next Door Arena, jijini Dar es Salaam.
 Mashabiki wa Liverpool wakishangilia kwa msisimko baada ya timu yao kutwaa Kombe la Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya sita, wapenzi wa kandanda zaidi ya 1,600 walijikusanya katika ukumbi wa Next Door Arena, jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad