HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 9, 2019

MATUKIO MBALIMBALI YA ZIARA YA DKT. MABODI SONGEA MJINI

 MLEZI wa CCM Mkoa wa Ruvuma Dk.Abdulla Juma Mabodi ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa akiwasili katika Wilaya ya CCM Songea Mjini kwa ajili ya ziara ya Kikazi ya kuimarisha Chama na Kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Wilaya hiyo.
 WAZEE wa Chama Cha Mapinduzi Songea Mjini wakimvisha Vazi la Heshima la Kimila la kumtambua Mlezi wa CCM Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu CCM Taifa kuwa ni Kiongozi Muadilifu aliyetambuliwa rasmi na Wazee wa Wilaya hiyo ambao ni Utaratibu wa Kimila uliasisiwa na Kiongozi Mkuu wa Kijadi ambaye ni Mzee Songea Mbano.
 MLEZI wa CCM Mkoa wa Ruvuma Dk.Abdulla Juma Mabodi ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa akiwa katika Kikao cha ndani na Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Songea  Mjini.
 WANACHAMA wapya waliojiunga na CCM wakila kiapo cha Uanachama mara baada ya kukabidhiwa Kadi za CCM na kupokelewa na Mlezi wa CCM Mkoa wa Ruvuma Dk.Abdulla Juma Mabodi ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM  Taifa huko katika Shina namba 4 Tawi la CCM Mtakuja na Kata ya Majengo Wilaya ya CCM Songea Mjini.
 WALIOKUWA Viongozi wandamizi wa CHADEMA waliojiunga na CCM na kupokelewa na Mlezi wa CCM Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Dk.Abdulla Juma Mabodi ambao ni Thimoth Tililo (kulia) aliyekuwa Mjumbe wa Mtaa wa Unangwa kupitia CHADEMA Wilaya ya Songea Mjini na aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CHADEMA Kata ya Misufini ndugu Juma Marwa Kionyori (kushoto) wakizzumgumza mara baada ya kujiunga na CCM na kupokelewa na Mlezi wa CCM Mkoa wa Ruvuma Dk.Abdulla Juma Mabodi.
MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Ruvuma Ndugu Oddo Killian Mwisho akizungumza katika Kikao cha ndani cha Viongozi na Watendaji wa Serikali kilichohitishwa na Mlezi wa CCM Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Dk.Abdulla Juma Saadalla 'Mabodi'.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad