HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 3, 2019

MAADHIMISHO YA MIAKA 55 YA MUUNGANO WA TANZANIA SAUDI ARABIA

Ubalozi wa Tanzania mjini Riyadh nchini Saudi Arabia iliadhimisha miaka 55 ya MUungano wa Tanzania kwa shuguli mbalimbali yakiwemo maonyesho ya utamaduni wa Mtanzania, vyakula vya asili ya Tanzania, utalii na bidhaa za kilimo na zinazozalishwa na viwanda vya Tanzania. 
Balozi Hemedi Mgaza akiwa pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi, Viongozi wa jumuiya ya watanzania waishio Riyadh wakiwapokea wageni waalikwa waliohudhuria siku hiyo.
Balozi Hemedi Mgaza akiwa na mgeni rasmi Meya wa Jiji la Riyadh Eng. Tariq Al Faris wakisimama kwa heshima wakati nyimbo za taifa za Tanzania na Saudi Arabia zikiimbwa.
Baadhi ya wakinamama Watanzania na wanadiaspora walioandaa sherehe za maadhimisho ya miaka 55 ya Muungano mjini Riyadh.
Wageni walikwa wakiwemo Watanzania wanaofanya kazi nchini Saudi Arabia na wanadiplomasia wakisikiliza hotuba wakati wa maadhimisho hayo.
Balozi wa Tanzania ncini Saudi Arabia Hemedi Mgaza akiwa na mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 55 ya Muungano wa Tanzania Meya wa Jiji la Riyadh Eng Tariq Al Faris wakikata keki kuzindua shere za maadhimisho.
 Wageni walikwa waliofika katika Ukumbi wa Utamaduni (Diplomatic Quarters Cultural Palace Hall) wakisikiliza hotuba ya Balozi iliyozungumzia kuitangaza Tanzania katika utalii, utamaduni, uwekezaji, masoko ya bidhaa za Tanzania na shughuli za madakatari wa hisani.
Mabalozi wawakilishai wa nchi za Cameroon, Nigeria na Ghana wakiwa na Balozi wa Tanzania wakionja vyakula vya asili ya Tanzania vilivyoandaliwa na Watanzania waishio Riyadh.
Baadhi ya bidhaa za utamaduni wa Tanzania zilizoonyeshwa wakati wa maadhimisho ya miaka 55 ya Muungano wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad