HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 30, 2019

DC AKATAA NYUMBA YA WALIMU YA MILION 52-SCRIPT PICHA NA SAUTI

 Na Ahmed Mahmoud Karatu
Mkuu wa wilaya ya Karatu Theresia Mahongo amegoma Kupokea Nyumba ya walimu ambayo inadaiwa kugharimu shilingi Milioni 52, zikiwa ni fedha kutoka kwa wafadhili milioni 34, nyingine zikitolewa na wananchi pamoja na serikali.

Mkuu wa Wilaya ya Karatu amefikia hatua hiyo wakati akipokea majengo mengine mawili ya bweni la Wanafunzi wa Kike pamoja na bwalo la Chakula yaliyojengwa na kwa ufadhili kutoka The African Foundations.
Huku akikaata nyumba ya walimu ya 3 in one ambayo imefadhiliwa na Serena hotel kwa madai fedha zilizotumika haziendani na uhalisia wa mradi. Katika mradi huo, Wananchi wameoa kiasi cha milioni Tisa, huku serikali ikitoa pia milioni Tisa kwaajili ya upauzi wa jengo.

Kwa upande wao wafadhili wa mradi huo wamekiri uwepo wa mapungufu hayo na kuahidi kuyafanyia Kazi.

Kuhusu msaada wa ujenzi wa Bweni la Wasichana pamoja na Bwalo la Chakula, Mkuu wa wilaya Mahongo amepongeza ujenzi huo, huku Meneja wa African Foundation, Mkomeni Ernest, amasema lengo ni kuhakikisha jamii inanufaika na uwepo wa makampuni yanayozunguka hifadhi zilizo karibu na wananchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad