HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 5, 2019

WACHINA, WATANZANIA NA WAZAMBIA WAADHIMISHA MIAKA 45 YA TAZARA

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Paramagamba Kabudi akihutubia katika siku ya kumbukumbu ya Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA, wakati wa zoezi la kuweka mashada ya maua iliyofanyika leo (Ijumaa April 5, 2019), katika makuburi ya mashujaa hao yaliyoko Gongo la Mboto Jijini Dar es Salaam, waliosimama kulia ni Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke akiwa pamoja na  viongozi kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Tanzania. 
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi (kulia), akipata maelezo kuhusu Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA, katika maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa hao yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa April 5, 2019), kushoto ni Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke akiwa pamoja na  viongozi wengine wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Tanzania. 
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi (kulia) na Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke (kushoto) wakiweka mashada ya maua katika moja ya makaburi ya Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA katika maadhimisho ya siku ya mashujaa hao iliyofanyika leo (Ijumaa April 5, 2019) Jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbasi akiweka maua kwatika  moja ya makaburi ya Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA, katika maadhimisho ya siku ya mashujaa hao iliyofanyika leo (Ijumaa April 5, 2019) Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi (kulia) na Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, wakiweka mashada ya maua katika mnara wa makaburi ya Mashujaa waliojenga Reli ya TAZARA, katika maadhimisho ya siku ya mashujaa hao iliyofanyika leo (Ijumaa April 5, 2019) Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi (kulia) na Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, wakitoa heshima mbele ya mnara wa makabuli ya Mashujaa waliojenga Reli ya TAZARA, katika maadhimisho ya siku ya mashujaa hao iliyofanyika leo (Ijumaa April 5, 2019) Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi, akionyesha maneno aliyoyaandika kuhusu maadhimisho ya siku ya mashujaa waliojenga reli ya TAZARA, katika siku ya kumbukizi iliyofanyika ijumaa hii katika makaburi ya mashujaa hao yaliyoko Gongo la Mboto Jijini Dar es Salaam, aliyesimama wa nne kushoto ni Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke akiwa pamoja na viongozi wengine wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Tanzania.
 Mnara wa Makabuli ya Mahujaa waliojenga Reli ya TAZARA yaliyoko Gongo la Mboto Jijini Dar es Salaam, kama unavyoonekana kwenye picha.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad