Na Shushu Joel, Chalinze.
MBUNGE wa jimbo la Chalinze, wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani
Kikwete ameendelea na ukamiloshaji wa ahadi zake alizokuwa amewaahidi
wananchi wa jimbo lake pindi alipokuwa akijinadi kuwaomba kura ili
aweze kuwasaidia kuwasemea bungeni ili serikali itatue changamoto
zao kwa wakati.
Maneno hayo alisema jana katika kijiji cha chahua kata ya Bwilingu
jimboni humo alipokuwwa akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa
zahanati ya kijiji hicho.
Akizungumza na wananchi wa eneo hilo mara baada ya uwekaji wa jiwe
la msingI Kikwete amewapongeza wananchi hao kwa usimamizi mzuri wa
fedha alizochangia katika ujenzi huo uligharimu zaidi ya milioni 40
mpaka sasa.
"Uwepo wa zahanati katika kijiji hiki utapunguza kama si kuondoa
kabisa vifo vya wazazi na watoto ambavyo sio vya lazima"Alisema
Kikwete.
Aliongeza kuwa wakati anawaomba wananchi hao ridhaa ya kuwa kiongozi
wao aliwahakikishia kabla ya miaka 5 kumalizika atahakikisha anajenga
zahanati katika kijiji hicho na hivyo jambo hilo limekamilika kwa
asilimia 90.
Aidha amewataka wananchi hao pindi zahanati hiyo itakapoanza kufanya
kazi wapendelee kupima afya zao ili kuweza kubainika nini
kinachokusumbua ili wataalamu waweze kubaini tatizo na kutatuliwa.

Hivyo mbunge huyo amewahakikishia wananchi wa jimbo hilo kuwa kila
alichokiahidi atatekeleza kabla ya miaka 5 kumalika cha msingi katika
mradI yote inayoletwa na serikali kwa ushawishi na ile mingine
inapaswa kulindwa ili itumike kwa vizazi vingi.
Kwa upande wake Fatuma Ally mkazi wa eneo hilo amempongeza mbunge kwa
jinsi anavyowapambania wananchi wa kijiji hicho katika kuhakikisha
wanapata maendeleo ya kila nyanja ili kuondokana na changamoto za
hapa na pale.
Aliongeza kuwa mbali na uwekaji wa jiwe la msingi katika zahanati hiyo
pia umetuletea umeme,kisima kikubwa cha maji na utengenezaji wa
miundombinu inayosaidia kurahisisha kwa shughuli za ufanisi wa
maendeleo katika maeneo yetu.
Aidha amempongeza Kikwete kwa jinsi alivyofanikisha ujenzi wa shule
ya msingi iliyokuwa to imechakaa kwa ujenzi wa madarasa matatu yenye
vyumba viwili viwili hivyo hali hiyo imssaidia kuchochea kwa
maudhurio mazuri ya watoto shuleni na kupata masomo yao ya kila siku.
Naye Abeid Salmu ambaye ni shehe wa msikiti wa kijiji hicho
amempongeza Kikwete kwa juhudi zake za ufanisi wa kuwaletea maendeleo
mbali mbali kwenye kijiji hicho bila kuchelewesha.
"Kijana wetu Ridhiwani a me kuwa akijituma sana katika uletaji wa
maendeleo hivyo tunamuomba aendelee utekelezaji huo huo kwa wananchi
wake"Alisema.
Aidha shehe huyo amemtoa wasiwasi mbunge huyo kuwa katika jimbo la
Chalinze hakuna mbunge mwenye moyo kama wake hivyo asijitokeze mtu
yeyote yule kuleta uso wake katika uchaguzi ujao kwani sie tunamjua
Kikwete ndio kimbilio letu kwani muda mchache tu kafanimisha mradI
mingi na mikubwa Chalinze.
No comments:
Post a Comment