VICTOR MASANGU, KIBAHA
VIJANA wapatao 35 katika halmashauri ya mji Kibaha iliyopo Mkoani
Pwani ambao walikuwa wanakabiliwa na wimbi la ukosefu wa upatikanaji
wa ajira wamepatiwa mafunzo maalumu ya ujasiriamali kwa lengo la
kuweza kujikwamua kiuchumi na kuondokana na tatizo la umasikini.
Hayo wamebainishwa na Meneja wa Taasisi ya ujasiramali na ushindani
Tanzania (TECC) Anna Manuti wakati wa ufunguzi rasmi wa mafunzo ya
siku 11 ya ujasiliamali kwa baadhi ya vijana waliopo katika
halmashauri ya mji Kibaha ambayo yameandaliwa kwa lengo la kuwapa
mbinu mbali mbali zitakazoweza kuwasaidia kujiajiri na kuacha na kuwa
tegemezi.
Aidha Meneja huyo amebainisha kuwa katika kukabiliana na changamoto
zinazowakabili baadhi ya vijana wameamua kuwakutanisha vijana hao kwa
lengo la kuwawezesha kwa kuwapatia elimu ambayo itawapa fursa ya
kuanzisha biashara zao wenyewe lengo ikiwa ni kujikwamua kiuchumi na
kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo.
“Hii programu ya kuwawezesha vijana mafunzo ya ujasiriamali tunaifanya
kwa kipindi cha miaka miaka mine na inatarajia kumalizika mwaka 2020
na kwa sasa huu ni mzunguko wa sita ambapo katika halmashauri ya
mji wa kibaha vijana wapatao 35 wamepata fursa ya kupatiwa mafunzo
haya ambayo yatawea kuwasaidia kuweza kujiajiri wao wenyewe,”alisema
Anna.
Kwa upande wake Meneja wa shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO)
Mkoa wa Pwani Behata Minga amesema programu ya kuwawezesha vijana
kwa kuwapatia mafunzo mbali mbali ya ujasiriamali itawasaidia vijana
kujiajiri wao wenyewe kutokana kuanzisha viwanda vidogovidogo lengo
ikiwa ni kujikwamua kiuchumi na kupambana na wimbi la umasikini.
“Kwa kweli mradi huu wa kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana
utaweza kuwa ni mkombozi mkubwa sana hasa katika Mkoa wetu wa Pwani na
sisis kama Sido tutahakikisha tunashirikiana bega kwa beda na taasisi
hii ya TECC ambayo imefanikisha kuwakusanya vijana hawa na kuwapa
mahalifa ambayo yatawasaidia kupata ajira pamoja na kuanzisha viwanda
vidogividogo,”alisema Mlinga.
Nao baadhi ya vijana ambao wameshiriki katika mafunzo hayo akiwemo
Selemani Shabani pamoja na Azaria Namga wamesema kwa sasa bado
wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo kutokuwa na ajira,
ukosefu wa mitaji ya biashara hivyo wameiomba serikali ya awamu
yatano kuwasaidia kwa halina mali ili kufanikisha malengo
waliyojiwekea.
MRADI huo wa kuwawezesha vijana kuwapatia mafunzo mbali mbali ya
ujasiriamali unatekelezwa katika mikoa mine ya Jiji la Dar es Salaam,
Dodoma, Mtwara pamoja na Pwani ambapo hadi sasa katika mikoa yote
hiyo vijana wapatao 894 wamenufaika na programu hiyo ambayo
inatarajia kumalizika mwaka 2020.
Meneja wa Taasisi ya ujasiramali na ushindani Tanzania
(TECC) Anna Manuti akizungumza jambo na vijana ambao wameshiriki
wakati wa ufunguzi rasmi wa mafunzo hayo ya ujasiliamali ambayo
yamefanyika katika katika kata ya maili moja Wilayani Kibaha.(PICHA NA
VICTOR MASANGU)
Meneja wa shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) Mkoa
wa Pwani Behata Minga akizungumza jambo katika ufunguzi wa mafunzo
ya ujasiliamali kwa vijana wa halmashauri ya mji Kibaha.(PICHA NA
VICTOR MASANGU)
Mmoja wa wawakilishi wa vijana kutoka katika halmashauri ya
mji Kibaha Shauri Yomba Yomba akizungumza na washiriki ambao hawapo
pichani kuhusiana na umuhimu wa mafunzo hayo ya ujasiriamali ambayo
yameandaliwa na taasisis ya TECC(PICHA NA VICTOR MASANGU)
Mwezeshaji wa semina hiyo ambaye pia ni Afisa kutoka
Shirika la kuhudumia viwanda vidogovidogo (SIDO) Mkoa wa Pwani Merina
Mkuchu akitoa maelekezo kwa vijana hao ambao wameshirki katika mafunzo
ya ujasiriamali.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
Baadhi ya vijana kutoka katika halmashauri ya mji Kibaha
ambao wameshiriki katika mafunzo ya ujasiriamali wakiwa wanasikiliza
mada ambazo zilizokuwa zikitolewa na wawezeshaji kutoka TECC pamoja na
SIDO.(PICHA NA VICTOR MASANGU.)
No comments:
Post a Comment