HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 15, 2019

RC MAKONDA AMUAGIZA MKURUGENZI ILALA KUITISHA KIKAO CHA DHARURA CHA BARAZA LA MADIWANI

*Aeleza kutofurahishwa na utekelezaji wa miradi Wilayani humo

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

KULEGALEGA na siasa chafu ya kukwamisha miradi ya maendeleo kwa makusudi kunakofanywa na baadhi ya Madiwani wa Wilaya ya Ilala, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam  Paul Makonda amemuagiza mkurugenzi wa manispaa hiyo kuitisha   kikao cha dharura cha Baraza la madiwani siku ya jumanne na endapo wajumbe watakaidi atalazimika kumpelekea Rais Magufuli mapendekezo ya kuvunja baraza hilo au kubadilisha mfumo kwa faida ya wananchi.

Makonda amesema kuwa inashangaza kuona serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais John Joseph Magufuli imekuwa ikitoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya utatuzi wa kero sugu za wananchi lakini baadhi ya wanasiasa wasiowatakia mema wananchi wamekuwa wakipinga miradi hiyo kwa makusudi na kupelekea wananchi kuona serikali yao haiwajali wakati tayari imeshatoa fedha za utatuzi wa kero zao.

Miongoni mwa miradi ambayo serikali imetoa pesa lakini zimeishia kubaki kwenye akaunti bila kutumika ni ujenzi wa machinjio ya kisasa vingunguti, ujenzi wa soko la kisutu na maboresho ya mto msimbazi ambao umekuwa ukisababisha athari za mafuriko kwa wananchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad