HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, April 27, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA BARABARA YA MBEYA-LWANJILO-CHUNYA KM 72 NA KUWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA CHUNYA-MAKONGOLOSI KM 39 CHUNYA MKOANI MBEYA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli, pamoja na viongozi mbalimbali Wabunge, Mawaziri, Viongozi wa Mkoa wa Mbeya, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mitambo itakayotumika katika ujenzi wa barabara ya Chunya hadi Makongolosi km 39 itakayojengwa kwa kiwango cha lami katika sherehe zilizofanyika Chunya mkoani Mbeya.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chhalamila mara baada ya kufungua barabara ya kutoka Mbeya-Lwanjilo-Chunya yenye jumla ya kilometa 72.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na viongozi wengine akivuta utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa barabara itakayojengwa kwa kiwango cha lami kutoka Chunya hadi Makongolosi km 39.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli, pamoja na viongozi mbalimbali Wabunge, Mawaziri, Viongozi wa Mkoa wa Mbeya, akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Barabara ya  Mbeya-Lwanjilo-Chunya yenye jumla ya kilometa 72 iliyokamika kujengwa kwa kiwango cha lami katika sherehe zilizofanyika Chunya mkoani Mbeya.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika uwanja wa Sabasaba Wilayani Chunya kwa ajili ya kuzungumza na wananchi katika mkutano wa Hadhara.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono kuwasalimia wananchi waliokusanyika katika uwanja wa Sabasaba Chunya kabla ya kuwahutubia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaDkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mhandisi Profesa Ninatubu Lema kutoka Wizara ya Ujenzi wakati alipowasili katika uwanja wa Sabasaba Chunya mkoani Mbeya. 




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Charangwa Chunya mkoani Mbeya wakati akielekea kufungua barabara ya Mbeya-Chunya-Lwanjilo km 72. 

PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad