HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 8, 2019

NEC yaungana na familia ya kumhifadhi marehemu Nanyaro kijijini kwao Arusha

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeungana familia, ndugu, jamaa na marafiki  kuuaga na kuuhifadhi kwenye makazi yake ya milele,  mwili wa mtumishi wake Clarence Nanyaro aliyefariki Aprili 2 mwaka huu na kuzikwa kijijini kwao Nkomaala, wilayani Meru mkoani Arusha.
Tume katika mazinshi hayo iliwakilishwa na Mkurugenzi Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Zanzibar, Felix Wandwe aliyeambatana na baadhi ya watumishi kumhifahdi marehemu Nanyaro aliyekuwa Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Habari wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura.
Akizungumza wakati akitoa salamu za rambirambi, Mkurugenzi Wandwe alisema Tume inaungana na familia, ndugu, jamaa na marafiki kuombeleza msiba wa mtumishi wake kwani marehemu Nanyaro alikuwa mtu wa kuaminiwa kutokana na utendaji kazi wake mzuri.
“Kwa niaba  ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi napenda kuwasilisha salamu za rambirambi kwa masikitiko makubwa.Marehemu alifanya kazi vizuri sana na tulimuamini na kumpenda, lakini kwa mapenzi ya  Mungu amemchukua, tunasema Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina lake lihimidewe” alisema Mkurugenzi Wandwe na kuongeza kuwa.
“Kuhusiana na suala la rambirambi napenda kueleza kwamba Ofisi inafanya utaratibu wa michango mbalimbali ambayo  baada ya hapa tutawasiliana na familia kujua utaratubu wa kuwasilisha.” “Pili kwa kuwa marehemu alikuwa mtumishi wa Serikali, kwa niaba ya Tume niseme kwamba zitafanyika taratibu za kisheria, kanuni na taratibu kuhusiana na stahiki zake na atapewa mtu kama sheria zinavyoelekeza”. 
Akitoa shukrani kwa niaba ya familia, Mkuu wa Boma Mzee Gadiel Nanyaro aliishukuru Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa huduma waliyoitoa kwa marehemu na kumuomba mwakilishi wake kufikisha shukrani hizo ofisini kutokana na ushirikiano mkubwa waliyoutoa kwa familia. Marehemu Nanyaro mbali na kufanya kazi Tume tangu mwaka 2015 hadi umauti unamkuta, pia alifanya kazi Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Shirika la Utangazaji (TBC) kwa nafasi mbalimbali.
Alifariki tarehe 2 Aprili mwaka huu kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na hivi karibuni alipata ‘Mild Stroke’ ambao ulisababisha alazwe kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa takribani siku 19 hadi umauti ulivyomkuta.
Akisoma akitoa salamu za rambirambi wakati watumishi wa Tume wakiaga mwili wa marehemu jijini Dar es Salaam, Mkugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura ya NEC, Giveness Aswile alisema alitoa shukrani za Tume kwa madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali ya Bochi kwa jitihada walizofanya katika kuokoa uhai wa marehemu.
“Tume inatoa shukrani kwa madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali ya Bochi kwa jitihada walizofanya katika kuokoa uhai wa marehemu.Pia inawashukuru viongozi wa dini, watu binafsi na taasisi mbalimbali kwa kumuhudumia marehemu wakati wa uhai wake.” alisema Mkurugenzi Aswile.

Marehemu ameacha mjane na watoto.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana lihimidiwe.
 Mkurugenzi Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Zanzibar, Felix Wandwe, akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Clarence Nanyaro, aliyezikwa mwishoni mwa juma hili kijijini kwao Nkomaala, wilayani Meru mkoa wa Arusha.
 Mjane wa Marehemu Clarence Nanyaro akiaga mwili wa marehemu
 Baba wa marehemu mzee Sabaya Nanyaro akiaga mwili wa marehemu mwanaye wakati wa ibada ya kuuaga mwili wa marehemu.
 Mkurugenzi Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Zanzibar, Felix Wandwe akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu.
 Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu.
 Baba na mama wa marehemu wakiwa an nyuso za huzuni wakati wa ibada ya kuuaga mwili wa marehemu.
 Baadhi ya waombolezaji waliohudhuria kumuaga marehemu Clarence Nanyaro, kwenye kijiji cha Nkomaala wilayani Meru mkoani Arusha.
 Baadhi ya waombolezaji waliohudhuria kumuaga marehemu Clarence Nanyaro, kwenye kijiji cha Nkomaala wilayani Meru mkoani Arusha.
 Baadhi ya waombolezaji wakishusha mwili wa marehemu kwenye kaburi lake.
 Baadhi ya watoto wa marehemu Clarence Nanyaro (wawili mbele) na mjane wa merehemu (kushoto aliyeshika kichwa) wakiwa kwenye majonzi wakati wa kuuaga mwili wa marehemu mpendwa wao.
 Mkurugenzi Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Zanzibar, Felix Wandwe, akimpa pole mjana wa marehemu Clarence Nanyaro an mtoto wake (kulia) baada ya kuuhifadhi mwili wa marehemu.
 Mkurugenzi Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Zanzibar, Felix Wandwe, akimpa pole baba wa marehemu mzee Sabaya Nanyaro.
 Mkurugenzi Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Zanzibar, Felix Wandwe, akimpa mkono wa pole mama wa marehemu Clarence Nanyaro.
 Mkurugenzi Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Zanzibar, Felix Wandwe, akiagana na Mkuu wa Boma, Mzee Gadiel Nanyaro baada ya kumaliza mazishi ya marehemu.
 Mkurugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura, Giveness Aswile wakati watumishi wa Tume walipouaga mwili wa mtumishi mwenzao Clarence Nanyaro katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi an waombelezaji wengine wakishiriki katika ibada ya kumuaga marehemu Clarence Nanyaro katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Picha na NEC

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad