HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 4, 2019

MRADI MKUBWA MAKAO YA TAIFA YA WATOTO DODOMA WAJA

Mradi Mkubwa wa Ujenzi wa Makao ya Watoto Dodoma wenye thamani ya dola za Kimarekani million 5.5 sawa na takriban Bilioni 10 za Kitanzania unatarajiwa kuanza hivi karibuni katika eneo la Kikombo nje kidogo ya Jiji la Dodoma katika eneo lenye ukubwa wa ekari 40.

Mradi huo ni wa kwanza na wa aina yake kwa kuwa tofauti na miradi mengine utakapokamilika utatoa huduma za utenganifu wa saikolojioa lakini pia utatoa elimu ya ufundi kuwawezesha watoto waishio katika mazingira magumu kupata stadi za kujitegemea na kuwezesha kaya maskini ambazo watoto hao wanatokea ili kukabiliana na umasikini wa familia.

Mradi huo Mkubwa unajengwa kwa Msaada wa Shirika la Kimataifa la Abbott lenye Makao yake Makuu Nchini Marekani na unajengwa Jijini Dodoma kufuatia Serikali kuhamishia Makao Makuu ya Serikali Jijini Dodoma hivyo kulazimika kuhamisha Makao ya Taifa ya Watoto ya Kurasini.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewataka wafadhili wakubwa wa Mradi huo kutoka Shirika la Abbott kuharakisha kuanza kwa Mradi huo mapema iwezekanavyo na kuhaidi kutoa ushirikiano wa kutosha kufanikisha zoezi la kuanza kwa Mradi huo.

‘’Anzeni Mradi huu kwa sasa kwa kuwa viongozi wote wako hapa Dodoma wakishiriki katika Bunge la Bajeti hivyo kuwa rahisi kutatua mambo kwa haraka maana mkichelewa baada ya Bunge la Bajeti watasambaa kila mahali kutekeleza shughuli nyingine za Serikali.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa Mradi huu unajengwa katika Jiji ambalo limepimwa tofauti na Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini ambayo kwa sasa yako katika msongamano wa makazi ambayo hayakupimwa jambo linalofanya Mradi huu kuwa wa aina yake hapa Nchini.

Aidha Dkt. Ndugulile ameishukuru Abbott Tanzania kwa kuanza kufadhili Wizara ya Afya kwa upande wa Maendeleo ya Jamii kwani Shirika hilo limekuwa Msaada mkubwa kwa upande wa Afya Tiba kwa kutoa Msaada katika vifaa vya tiba na huduma za dharula katika hospitali.

Akitoa ufafanuzi wa Mradi huo kwa Naibu Waziri Ndugulile Kamishina wa Ustawi wa Jamii Nchini Dkt. Naftal Ng’ondi amesema tayari Serikali ya Mkoa wa Dodoma imetoa eneo la ekari 40 kwa ajili ya ujenzi huo na kichosubiriwa kwa sasa ni kibali cha ujenzi wa Makao hayo mapya ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu.
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akijadiliana jambo na Makamu wa Rais wa Mfuko wa Abbott Tanzania Bw.Andy Wilson pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko huo Natalia LoBue walipofika Ofisini kwake kumpa taarifa ya Mradi wa Ujenzi wa Makao mapya ya Taifa ya Watoto yanayotarajiwa kujengwa hivi karibuni Jijini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akijadiliana jambo na Makamu wa Rais wa Mfuko wa Abbott Tanzania Bw.Andy Wilson pamoja na Kamishna wa Ustawi wa Jamii Nchini Dkt. Naftal Ngo’ndi wa kwanza kushoto walipofika Ofisini kwake kumpa taarifa ya Mradi wa Ujenzi wa Makao mapya ya Taifa ya Watoto yanayotarajiwa kujengwa hivi karibuni Jijini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akijadailiana jambo na Ujumbe wa Mfuko wa Abbott Tanzania ulipofika Ofisini kwake kumpa taarifa ya Mradi wa Ujenzi wa Makao mapya ya Taifa ya Watoto yanayotarajiwa kujengwa hivi karibuni Jijini Dodoma.
 Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu akijadiliana jambo na Makamu wa Rais wa Mfuko wa Abbott Tanzania Bw.Andy Wilson alipofika Ofisini kwake pamoja na ujumbe wake kumpa taarifa ya Mradi wa Ujenzi wa Makao mapya ya Taifa ya Watoto yanayotarajiwa kujengwa hivi karibuni Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. Dkt. John Jingu akijadiliana jambo na Ujumbe wa Mfuko wa Abbott Tanzania ulipofika Ofisini kwake kumpa taarifa ya Mradi wa Ujenzi wa Makao mapya ya Taifa ya Watoto yanayotarajiwa kujengwa hivi karibuni Jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad