Na Anthony Ishengoma
Kamati ya Uwezeshaji Wanawake katika Umiliki na Matumizi ya Ardhi inakaa leo Jijini Dodoma kujadili na kuhainisha fursa na vikwazo vya kuwezesha umiliki wa ardhi kwa wanawake na kupanga mikakati ya kufikia lengo la wanawake kumiliki na kutumia ardhi kwa maendeleo yao.
Akifungua Kikao cha Kamati hiyo mapema leo Jijini Diodoma Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Patrick Golwike amewaambia wajumbe wa kamati hiyo kuwa kikao hicho ni muhimu kwa kuwa kinajaadili namna bora ya kuwawezesha wanawake kumiliki na kutumia ardhi katika kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Aidha Golwike ameongeza kuwa pamoja na kuwepo kwa sheria na jitihada mbalimbali kutoka kwa wadau wa kusaidia wanawake kunufaika na ardhi bado kuna vikwazo vinavyoathiri wanawake kumiliki ardhi kwa sababu mbalimbali zikiwemo mila na desturi, ufahamu mdogo wa umiliki ardhi ikiwemo ukosefu wa dhamana za kiuchumi.
Golwike amewataka wajumbe wa kamati hiyo kupitia kwa Taasisi wanazotoka kuwa wabunifu wakwenda na ubunifu wa sayansi na teknolojia katika kuwawezesha wanawake kumiliki na kutumia ardhi kama njia ya kujikwamua kiuchumi.
Akitoa ufafanuzi kwa vyombo vya habari vilivyotaka kujua hasa lengo la Kamati hiyo ndogo ya Ardhi Mkurugenzi wa Idara ya Jinsia wa Wizara ya Afya Idara Kuu Maeandeleo ya Jamii Julius Mbilinyi amesema kuwa Kamati hii iliundwa ili kufikia Malengo Endelevu na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano kwa kuhakikisha wanawake wanapata fursa ya kumiliki ardhi na kuitumia kujiletea maendeleo.
Aidha Mbilinyi ameongeza kuwa kamati ndogo ya ardhi imejiwekea mikakati ya kuhakikisha wanawake wanaondokana na vikwazo vya muda mrefu kama vile mila na desturi ili waweze kutumia fursa ya kumiliki ardhi na kuitumia kujiendeleza kiuchumi na kuwa Sehemu ya uchumi mpana wa Nchi yetu.
‘’Suala kubwa sio umiliki wa ardhi kwa wanawake lakini pia ni kuangalia namna bora wanawake hawa wanaitumia fursa ya mali hisa ya ardhi kujiletea maendeleo ili wawe sehemu ya uchumi mpana wa Taifa letu”. Aliongeza Mbilinyi.
Wakati huohuo Marry Ndalo kutoka Shirika la Kimataifa la Care ameongeza kuwa Kamati hiyo kimsingi inawakutanisha wadau kutoka Mashirika yasiyo ya Kiserikali na kuwaweka pamoja kujadiliana masuala ya ardhi lakini pia kupata taarifa kuhusu idadi ya Wanawake wanaomiliki ardhi na wasio miliki ardhi ili kuweka wanawake katika mjadala wa ardhi ambao inaajiri wanawake wengi.
Kaimu
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Patrick Golwike
kulia pamoja na Mwakilishi kutoka Shirika la Kimataifa la Care Marry
Ndalo wakiwa tayari kwa ufunguzi wa kikao cha Kamati Ndogo ya Ardhi
kujadili suala la umiliki wa ardhi kwa wanawake mapema leo Jijini
Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Jinsia wa Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya
Jamii Julius Mbilinyi kushoto pamoja na Mwakilishi kutoka Shirika la
Kimataifa la Care Marry Ndalo wakiwa tayari kwa ufunguzi wa kikao cha
Kamati Ndogo ya Ardhi kujadili suala la umiliki wa ardhi kwa wanawake
mapema leo Jijini Dodoma.
Picha
ya pamoja ya Kamati ndogo ya Ardhi mara baada ufunguzi wa kikao cha
Kamati Ndogo ya Ardhi kujadili suala la umiliki wa ardhi kwa wanawake
kilichofanyika katika ofisi mpya za Wizara ya Afya zilizoko Mtumba
Jijini Dodoma.
Baadhi
ya Washiriki wa Kamati ndogo ya Ardhi inayokutana leo Jijini Dodoma
kujadili suala la umiliki wa ardhi kwa wanawake katika ukumbi wa Wizara
ya Afya Mtumba Jijini Dodoma.
No comments:
Post a Comment