HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, March 22, 2019

Ubalozi wa Uswizi wazindua awamu ya tatu ya progamu ya uwajibikaji wa Kijamii

UBALOZI wa Uswisi nchini Tanzania kupitia shirika la Maendeleo ya Ushirikiano la Uswisi SDC umezindua awamu ya tatu ya programu ya uwajibikaji wa kijamii (Social Accountability Programme SAP).

ASAP inachangia kuziwezesha asasi za kiraia (AZAKI) zinazofanya kazi ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania na kusaini mkataba huo wa pamoja

  Balozi wa Switzerland nchini Tanzania Florence Tinguely Mattli  amesema, nchi yao ina nia ya kuchangia zaidi katika kuimarisha utendaji kazi na uwajibikaji wa mamlka za umma ili zitoe huduma bora kwa wananchi.

Amesema, SDC itachangia bilion 18 kwa kipindi cha miaka minne ijayo kwa asasi kadhaa za kiraia ikiwa ni pamoja na Foundation for Civily Society (FCS), Policy Forum na Twaweza na zitashirikiana na asasi hizi ambazo zinahusika na uanzishwaji na usimamizi wa sera za maendeleo ili kuboresha maisha ya wananchi ya kawaida.

“Uswisi tunaamini kwamba asasi za kiraia ni moja a wadau muhimu kwa nchi ya Tanzania ili kufikia malengo yake ya dira ya maendeleo ya Taifa 2025, na ASAP ni sehemu ya michango katika kuimarisja masuala ya uwajibikaji ikiwa na uhusiano wa muda mrefu na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kwenye kuimarisha uwezo wake wa uchunguzi,”amesema 

Kwa upande wa Mkurugenzi Aidan Eyakuze amesema kuwa, mradi huu utazidi kuimarisha uwazi kwa wananchi na taifa  na umuhimu wa kushirikiana na wananchi na kuhakikisha sauti zao zinasikika kwenye kutunga na kuboresha sera zinazowahusu wao.

Ameeleza kuwa, uwajibikaji katika kuleta maendeleo , ubunifu na utekelezaji wa kutathmini maendeleo ya wananchi.

Mweyekiti wa FCS Francis Kiwangwa ameongezea kwa kusema Mradi huu utasaidia katika ufuatiliaji wa rasilimali, kuimarisha mifumo ya udhibiti rasilimali pamoja na uwazi na uwajibikaji.


Uswisi imekuwa ikichangia miradi mbalimbali ya maendeleo nchini tangu mwaka 1960 na inaendelea kutoa takriban bilioni 51 kila mwana kusaidia sekta ya afya, ajira na mapato na utawala bora.
Balozi wa Switzerland nchini Tanzania Florence Tinguely Mattli(kulia)  akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla fupi ya kutiliana sahihi wa shilingi bilioni 18 kwa asasi za Kiraia(AZAKI) kupitia Shirika la Maendeleo na Ushiriano wa Uswisi (SDC) ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze.
Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society Francis Kiwanga akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wanavyofanya kazi na asasi zaidi ya 150 ya hapa nchini ili kuhimarisha ufuatiliaji wa raslimali wakishiriana na Serikali pamoja na wadau wengine kama Ubalozi wa Switzerland nchini Tanzania. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze na kulia ni Balozi wa Switzerland nchini Tanzania Florence Tinguely Mattli.
Mwenyekiti wa Mtandao Policy Forum, Japhet Makongo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna wananchi wanavyoweza kutoa maoni kwa kuunganisha sauti ya mtu mmoja mmoja au vikundi kupitia mtandao huo wakati wa hafla fupi ya kutiliana sahihi wa shilingi bilioni 18 kwa asasi za Kiraia(AZAKI) kupitia Shirika la Maendeleo na Ushiriano wa Uswisi (SDC). Kulia ni Mkuu wa Ushirikiano wa Ubalozi wa Switzerland nchini Tanzaania Romana Tedeschi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze(katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taasisi hiyo inavyofanya kazi kwa ushirikiano na Ubalozi wa Switzerland nchini Tanzaania wakati wa hafla fupi ya kutiliana sahihi wa shilingi bilioni 18 kwa asasi za Kiraia (AZAKI). Kulia ni Balozi wa Switzerland nchini Tanzania Florence Tinguely Mattli na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society Francis Kiwanga.
Balozi wa Switzerland nchini Tanzania Florence Tinguely Mattli(katikati) akifuatilia utiliaji saini wa awamu ya Tatu ya programu ya uwajibikaji wa Kijamii(Social Accountability Programme- SAP) baina ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze(kushoto) na Mkuu wa Ushirikiano wa Ubalozi wa Switzerland nchini Tanzania Romana Tedeschi(kulia) ili kuziwezesha asasi za kirai(AZAKI) ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania. 
Balozi wa Switzerland nchini Tanzania Florence Tinguely Mattli(wa pili kulia) akifuatilia utiliaji saini wa awamu ya Tatu ya programu ya uwajibikaji wa Kijamii(Social Accountability Programme- SAP) baina ya Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society Francis Kiwanga(wa pili kushoto) na Mkuu wa Ushirikiano wa Ubalozi wa Switzerland nchini Tanzania Romana Tedeschi(kulia) ili kuziwezesha asasi za kirai(AZAKI) ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania.

 Balozi wa Switzerland nchini Tanzania Florence Tinguely Mattli(wa pili kulia) akifuatilia utiliaji saini wa awamu ya Tatu ya programu ya uwajibikaji wa Kijamii(Social Accountability Programme- SAP) baina ya Mwezeshaji wa Mtandao Policy Forum, Semkae Kilonzo(wa pili kushoto) na Mkuu wa Ushirikiano wa Ubalozi wa Switzerland nchini Tanzania Romana Tedeschi(kulia) ili kuziwezesha asasi za kirai(AZAKI) ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania. wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Mtandao Policy Forum, Japhet Makongo.

Balozi wa Switzerland nchini Tanzania Florence Tinguely Mattli(katikati) akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society Francis Kiwanga(kushoto)  mara baada ya utiliaji saini wa awamu ya Tatu ya programu ya uwajibikaji wa Kijamii(Social Accountability Programme- SAP)  ili kuziwezesha asasi za kirai(AZAKI) ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania. 
Balozi wa Switzerland nchini Tanzania Florence Tinguely Mattli(wa pili kulia) akimpongeza Mwenyekiti wa Mtandao Policy Forum, Japhet Makongo(kushoto)  mara baada ya utiliaji saini wa awamu ya Tatu ya programu ya uwajibikaji wa Kijamii(Social Accountability Programme- SAP)  ili kuziwezesha asasi za kirai(AZAKI) ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania. 

Mkutano ukiendelea

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad