HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 7, 2019

Profesa Kabudi akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Dkt. Richard Sezibera. Katika mazungumzo yao,Sezibera alimpongeza  Prof. Kabudi kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mazungumzo hayo yalihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Ernest Mangu na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Wilbroad Kayombo. Sezibera yupo nchini kwa ajili ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Rwanda,  Paul Kagame. 
Balozi wa Rwanda nchini Tanzania,  Eugene Kayihura (kulia) na Afisa Ubalozi wa Rwanda wakifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Kabudi na  Dkt. Sezibera (hawapo pichani). 
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi akimwelezea jambo Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Dkt. Richard Seziberawakati wa mazungumzo hayo.
Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda,  Ernest Mangu pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Bw. Wilbroad Kayombo wakiwa kwenye Mazungumzo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Prof. Palamagamba Kabudi (katikati) pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda,  Dkt. Richard Sezibera (wapili kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Ernest Mangu (wa kwanza kulia) na Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, Eugene Kayihura (wa kwanza kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo yao. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad