HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, March 3, 2019

BONANZA LA KUPINGA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI LAFANA KIGOMA

WAZIRI wa elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amefungua na kushuhudia bonanza la mpira wa miguu kwa watoto kike wa shule za msingi, Sekondari na vyuo lililofanyika katika Wilaya Kasulu Mkoani Kigoma huku likiwa limemebea ujumbe wa Mimba na ndoa utotoni basi, Elimu ni haki yangu.

Akizungumza katika bonanza hilo Prof. Ndalichako amesema kuwa masuala ya mimba na ndoa utotoni zisiwe sababu za watoto kukatisha masomo yao, na ameitaka jamii kuhakikisha tamaduni hizo zinakufa mara moja na kila mmoja awe na wajibu wa kuhakikisha watoto wa kike wanatimiza malengo yao kielimu.

Amesema kuwa mpango wa Serikali kutoa elimu bure kwa wote umelenga watoto wote wanufaike na mpango huo  na kueleza kuwa Serikali haitawafumbia macho wale wote wanaokatisha masomo kwa watoto wa kike kwa namna yoyote ile.

Katika mashindano hayo zawadi mbalimbali zilitolewa kwa washiriki zikiwemo fedha taslimu pamoja na vyeti, washindi walioibuka katika bonanza hilo ni pamoja na Chuo cha Ualimu Kabanga, chuo cha F.D.C, Kinkati sekondari na chuo T.T.C Kasulu.

Pia timu zote zilizoshiriki mashindano hayo zilipata jezi, mipira, vifaa ya shule,taulo za kike huku wanafunzi wa chuo cha uwalimu Kasulu wakiondoka na kombe baada ya kuongoza katika mashindano hayo, wakifuatiwa na Murusi, Kinkati, Murubona sekondari, Muka sekondari, Kasulu F.D.C, Bogwe Sekondari na Kabanga TC.

Bonanza hilo liliandaliwa na mwakilishi wa umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) Mariam Ntakisivya na mashindano hayo kuitwa (Mariam Cup) kwa UWT Mkoa wa Kigoma.
 Waziri wa elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza wakati wa kufungua bonanza la mpira wa miguu kwa watoto kike wa shule za msingi, Sekondari na vyuo lililofanyika katika Wilaya Kasulu Mkoani Kigoma huku likiwa limemebea ujumbe wa Mimba na ndoa utotoni basi, Elimu ni haki yangu. Kushoto ni Mwakilishi wa umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) Mariam Ntakisivya mwanzilishi wa bonanza hilo.
Mwakilishi wa umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) na muandaaji wa Bonanza hilo Mariam Ntakisivya  akizungumza na waandishi wa habari wakati wa  bonanza la mpira wa miguu kwa watoto kike wa shule za msingi, Sekondari na vyuo lililofanyika katika Wilaya Kasulu Mkoani Kigoma huku likiwa limemebea ujumbe wa Mimba na ndoa utotoni basi, Elimu ni haki yangu.
Waziri wa elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akipiga mpira kuashiria ufunguzi rasmi wa bonanza la mpira wa miguu kwa watoto kike wa shule za msingi, Sekondari na vyuo lililofanyika katika Wilaya Kasulu Mkoani Kigoma huku likiwa limemebea ujumbe wa Mimba na ndoa utotoni basi, Elimu ni haki yangu.
Baadhi ya timu za watoto wa kike wa shule za msingi, Sekondari na vyuo  wakiwa kwenye maandalizi ya mwisho ya bonanza hilo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad