HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, March 8, 2019

AKUTWA AMEFARIKI DUNIA KWENYE KORONGO LA MAJI

Anaandika Dixon Busagaga.Hai.

MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Diamon Munishi (87) amekutwa amefariki dunia katika Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.

Kwa mujibu wa mashuhuda wameeleza kuwa marehemu alikua na tatizo la uoni hafifu na kwamba alianguka kwenye korongo wakati mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali ikinyesha.

Mkuu wa Polisi wilaya ya Hai Lwelwe Luhaga Mpina alithibitisha kufariki dunia na kwamba kifo chake ni cha kawaida kutokana na  matatizo aliyokuwa nayo marehemu.

Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya alifika eneo la tukio na kutoa pole kwa familia iliyofikwa na msiba wa mzee wa huyo.
 Mwili wa Daimon Munishi ukitolewa kwenye Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.
 Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya (mwenye kofia) alitizama mwili uliokutwa katika Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.
 Mwili wa Daimon Munishi ukipandishwa kwenye gari la polisi mara baada ya kutolewa kwenye Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.
 
Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya ( mwenye kofia) akitoa pole kwa wananchi waliofika eneo la tukio wakati wa kutoa mwili wa marehemu kwenye Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.
 Katibu tawala wilaya ya Hai,Upendo Wera akitoa pole kwa wananchi wa eneo hilo

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad