HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, February 24, 2019

Wasabato Bagamoyo watakiwa kushirikiana


Na Sophia Mtakasimba , Bagamoyo

WAUMINI wa kanisa la Waadventista Wasabato Bagamoyo wametakiwa kufanya kazi ya kushirikiana ili kuweza kusaidia kazi ya Mungu kusonga mbele na kuwafikia  watu wengi.

Wito huo umetolewa na Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Mashariki kati mwa Tanzania , Mchungaji Joseph Mngwabi ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa sherehe ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Kanisa jipya la kisasa la Waadiventista wasabato Bagamoyo uliofanyika jana (jumamosi) wilayani Bagamoyo mkoani Pwani .

“Mkifanya kazi kwa kushirikiana na kwa lengo moja ,mtafanikiwa sana kufikia malengo mliyojiwekea na hii itasaidia sana kufanya kazi ya Mungu isonge mbele”alisema Mchungaji Mngwabi.

Awali katika hotuba ya kumkaribisha mgeni rasmi Mchungaji wa mtaa wa Bagamoyo Mch.Melkizedeki Wanjala, alisema kuwa kanisa la Waadventista Wasabato Bagamoyo lilitengwa kuwa Kanisa kutoka Kanisa mama la Mwenge mnamo  mwaka 1995,ambapo hadi kufika mwaka 2001  Kanisa lilifanikiwa kuwa wa jengo lake la kuabudia eneo la Tandika-Bagamoyo. Lakini kufikia mwaka 2013 idadi kubwa ya waumini iliongezeka,hali hii ilipelekea jengo la awali kutotosha ,hivyo kuwa na hitaji la kuwa na Kanisa kubwa zaidi.

Akizungumzia ujenzi wa jengo jipya la Kanisa Mchungaji Wanjara amesema kuwa jengo hilo litagharimu jumla ya Shilingi za kitanzania Milioni Mia Nne na Hamsini (450,000,000) hadi kukamilika kwake ,hivyo amewataka washiriki kushirikiana kwa hali na mali  ili kukamilisha ujenzi huo huku akinukuu Maandiko Matakatifu kutoka kitabu cha Kutoka 25:8 yanayosema “nao wanifanyie patakatifu ili nipate kukaa kati yao.
Askofu wa Kanisa la Waadventista wa Sabato Jimbo la Mashriki Kati mwa Tanzania ,Mchungaji Joseph Ngwambi(Kushoto) , akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kanisa la Waadventista wa Sabato Bagamoyo, Kulia ni wa Jimbo la mashariki kati mwa Tanzania Ndg.Enock Rabieth .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad