HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, February 13, 2019

Upelelezi kesi ya Wema umekamilika


Na Karama Kenyunko
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imesema Februari 21, mwaka huu itamsomea  maelezo ya awali (PH) msanii wa Filamu nchini,  Wema Sepetu anayekabiliwa na shtaka moja la kuchapisha video ya ngono na kusambaza katika mitandaoni ya kijamii.

Hatua hiyo imefikiwa leo Februari 13, 2019 baada ya Wakili wa Serikali, Glori Mwenda kuieleza mahakama kuwa, upelelezi wa shauri hilo umekamilika na kuimba mahakama kupanga tarehe ya kumsomea mshtakiwa huyo PH.
Kufuatia taarifa hiyo Hakimu Mkazi, Maira Kasonde, ameiahirisha kesi hiyo mpaka Februari 21, mwaka huu.

Wema ambaye alikuwa Miss Tanzania mwaka 2006,
anatetewa na Wakili, Ruben Simwanza, alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Novemba Mosi, 2018, kujibu shtaka hilo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad