HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, February 18, 2019

RAIS DKT SHEIN AENDELEA NA ZIARA YAKE WILAYA KASKAZINI A UNGUJA

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar. Mhe Riziki Pembe Juma, baada ya kuweka jiwe la Msingi la Skuli ya Sekondari ya Kijini Matemwe Wilaya ya Kaskazini 'A' Unguja, leo.lililojengwa na Kampuni ya And Beyond Island Lodge ya Hoteli ya Mnemba, hafla hiyo imefanyika katika eneo la Skuli hiyo Kijini Matembe.(Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akielekea sehemu iliotengwa kwa ajili ya kuzungumza na Wananchi wa Kijiji cha Kijini na Mbuyu Tende, baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Skuli ya Sekondari ya Kijini Matemwe Wilaya ya Kaskazini 'A' Unguja.(Picha na Ikulu)
 /WANANCHI wa Vijiji vya Kijini na Mbuyu Tende Wilaya ya Kaskazini 'A' Unguja wakiwa katika viwanja Skuli ya Kijini Matemwe wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Skuli ya Sekondari ya Kijini Matemwe.(Picha na Ikulu)
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar.Bi. Madina Mjaka,akizungumza na kutoa Taarifa ya Kitaalamu ya Ujenzi wa Madarasa ya Skuli ya Sekondari ya Kijini Matemwe Wilaya ya Kaskazini 'A' Unguja, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Skuli hiyo, uliofanyika leo.17-2-2019.(Picha na Ikulu)
 WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar.Mhe. Riziki Pembe Juma, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Madarasa ya Skuli ya Sekondari ya Kijini, uliofanyika katika viwanja vya Skuli hiyo, kabla ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohemed Shein, kuwahutubia Wananchi wa Jimbo la Kijini Wilaya ya Kaskazini 'A'Unguja,LEO 17-2-2019.(Picha na Ikulu)
 MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akizungumza wakati wa hafla hiyo ya ufunguzi wa Skuli ya Sekondari ya Kijini Matemwe Wilaya ya Kaskazini 'A'Unguja, kushoto Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, na kushoto Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar.Dr. Abdallah Juma Mabodi.(Picha na Ikulu)
 MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Viongozi wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja alipowasili katika viwanja vya Hoteli ya Lagema Nungwi kuzungumza na Wanachama wa CCM wa Wilaya ya Kaskazini 'A'Unguja akiwa katika ziara yake ya kutembelea Miradi ya Maendeleo ya Wilaya ya Kaskazini A Unguja leo.17-2-2019.(Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akielekea katika ukumbi wa mkutano katika Hoteli ya Lagema Nungwi, kulia Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Vuai Mwinyi na kushoto Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini UngujaNdg. Iddi Ali Ame.(Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi wa meza kuu wakiwa wamesimama wakati ukiimbwa wimbo wa "Sisi Sote Tumegomboka" alipowasili katika ukumbi wa Hoteli ya Lagema, kuzungumza na Wanachama wa CCM wa Wilaya ya Kaskazini "A" Unguja, akiwa katika ziara yake Mkoa wa Kaskazini Unguja, leo 17-2-2019.(PIcha na Ikulu)
 WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Unguja wakiwa katika ukumbi wa hoteli ya Lagema Nungwi wakiimba wimbo wa "Sisi Sote Tumegombioka" wakati wa kuwasiliu Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, kuzungumza na Wanachama wa CCM wa Wilaya ya Kaskazini "A"Unguja leo.17-2-2019.(Picha na Ikulu)

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.,Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wanachama wa CCM wa Mkoa wa Kaskazini Unguja katika ukumbi wa Hoteli ya Lagema Nungwi leo, akiwa katika ziara yake.(Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad