HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, February 24, 2019

MTENDAJI MKUU TEMESA ZIARANI MIKOA YA IRINGA, NJOMBE, MBEYA, RUKWA NA KATAVI

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akikagua mojawapo ya mashine iliyopo katika karakana ya wakala huo mkoa wa Njombe wakati wa ziara yake ya kukagua utendaji kazi, kushoto ni Kaimu Meneja wa Temesa Mkoa wa Njombe Mhandisi Saidi Mawazo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akiichunguza mashine ya kuchongea vipuri vya mitambo mbalimbali wakati akikagua chumba cha kuhifadhia mashine hizo katika karakana ya mkoa wa Mbeya. Kulia ni Meneja wa TEMESA mkoani humo Mhandisi Sunday Kyungai.
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mkoa wa Katavi Mhandisi Stembrige Rushatila katikati akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Mhandisi Japhet Y. Maselle kushoto eneo la karakana wanapotegemea kupaboresha ili kuongeza uzalishaji wakati wa ziara ya mtendaji mkuu kukagua miundombinu ya karakana za wakala.  
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mkoa wa Iringa Mhandisi Ian Makule kulia akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Mhandisi Japhet Y. Maselle mashine ya kisasa ya kutoa na kubadilishia matairi ya magari iliyopo katika karakana ya mkoa huo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa TEMESA mkoa wa Iringa mara baada kuzungumza nao na kusikiliza changamoto wanazokutana nazo katika utendaji kazi. Kulia kwake ni Meneja wa TEMESA Mkoani humo Mhandisi Ian Makule.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akitoa msisitizo wakati akizungumza na wafanyakazi wa wakala huo mkoani Rukwa alipokua ziarani kukagua utendaji kazi. Pembeni yake ni Meneja wa Mkoa huo Mhandisi Fidol Tumbi.PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO - (TEMESA)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad