HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, February 24, 2019

KATIBU WA ACT WAZALENDO NA WENZAKE 162 WAJIUNGA CCM WILYANI MUFINDI ,WASEMA JPM ANATOSHA



Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa,Dkt.Abel Nyamahanga akipokea bendera ya chama cha ACT wazalendo kutoka kwa Ambi Daudi ambae ni Katibu wa ACT wazalendo wilaya ya Mufindi aliyejiunga na CCM leo hii katika maadhimisho ya miaka 42 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi ccm.

……………………………………………………………

Maadhimisho hayo yamefanyika kwa wilayani Mufindi kwa kushiriki katika shughuli za kijamii huku Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa akishirikiana na Kaimu katibu wa CCM Mkoa Marco Mbaga,Mkuu wa wilaya ya Mfindi Jamhuri David pamoja,Wabunge pamoja na viongozi wa ccm wilaya ya Mufindi,wanachama na wananchi,wameshiriki madhimisho hayo kwa kuchimba msingi wa ujenzi wa vyoo mbora katika shule ya sekondari Upendo,kujenga daraja,kukabidhi mifuko 49 ya saruji kwa kikundi cha vijana wajasilimali wanaojishughuliisha na utengenezaji wa tofali katika eneo la soko la Mafinga Mjini na shule ya sekondari upendo kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vyoo pamoja pia wamezungumza na walimu wa wilaya ya Mufindi.

Katika maadhimisho hayo jumla ya wanachama wapya 162 wamejiunga na chama cha mapiduzi ccm,na kusema kuwa wamekunwa na utendaji mzuri wa Rais Magufuli.PICHA NA ESTA MALIBICHE
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Dkt. Abel Nyamahanga akivalishwa skafu mara baada ya kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Mufindi leo asubuhi.

Badhi ya wanachama wapya waliojiunga na chama cha mapinduzi CCM leo katika maadhimisho ya miaka 42 ya kuzaliwa CCMm,yaliyoadhimishwa wilayani humo.


Kiongozi wa soko la Mafinga akipokea mifuko ya saruji kwa ajili ya kikundi cha vijana wajasiliamali wanaojishughulisha na utengenezaji wa tofali.

Mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Iringa Dkt.Abel Nyamahanga pamoja na Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wilium wakichimba msingi kwa ajili ya ujenzi wa vyoo bora katika shule ya sekondari Upendo iliyopo Mafinga Mjini.

Mbunge wa Mufindi Kusini Mendrad Kigola akichimba msingi kwa ajili ya ujenzi wa vyoo bora katika shule ya sekondari Upendo iliyopo Mafinga Mjini.





Ujenzi wa daraja katika kata ya Upendo Mfinga mjini zikiendelea







No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad