Na Ripota Wetu
KLABU ya Soka ya Juventus wanajipanga kutoa kitita cha pauni milioni 175 ili
kumsajili mshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri Mohamed Salah(26).
Taarifa kuhusu Juventus kujiandaa kumsajili mchezaji huyo wa Liverpool ambaye
kwa sasa yupo kwenye ubora zinatokana na tetesi ambazo zimebainika kuwepo kwa
mpango huo.
Wakati kukiwa na tetesi hizo, pia tetesi nyingine katika anga la soka zinaeleza kuwa
hatma ya Maurizio Sarri kama kocha wa Chelsea utaamuliwa ndani ya wiki mbili
zijazo.Tetesi hizo ni kwa mujibu wa Telegraph.
Hata hivyo wakati ikisubiriwa hatma ya kocha huyo, inaelezwa kuwa wachezaji wa
Chelsea walifanya kikao maalum cha 'kurekebishana' katika uwanja wao wa mazoezi
wa Cobham jana Jumatatu kutokana na kipigo walichopata cha 6-0 dhidi ya
Manchester City. (Mail)
Naye Kocha wa Derby Frank Lampard amepuuzia uvumi kuwa huenda akarithi
mikoba ya Maurizio Sarri endapo Chelsea itaamua kumfukuza. (Evening Standard)
Wakati huo huo kuna tetesi zinaeleza kuwa Beki wa Tottenham Juan Foyth mwenye
umri wa miaka 21 amefichua kuwa alikataa kujiunga na klabu ya Paris Saint-
Germain ili ajiunge na Spurs mwaka 2017. Tetesi za beki huyo zimetolewa na Goal.
Tetesi nyingine kwenye soka zinadai kuwa Barcelona wamefikia makubaliano na
klabu ya Eintracht Frankfurt kumsajili streka wao raia wa Serbia Luka Jovic, 21,
mwishoni mwa msimu. (Diario Sport)
Wakati mshambuliaji wa Juventus raia wa Argentina Paulo Dybala, 25, anakaribia
kufikia makubaliano ya kuhamia Real Madrid mwishoni mwa msimu. (AS)
Kwa upande wa Manchester United wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili
kiungo wa Paris Saint-Germain Adrien Rabiot(23) mwishoni mwa msimu. (AS - via
Mirror).
No comments:
Post a Comment