HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 26, 2019

BENKI YA NMB YADHAMINI MKUTANO WA WADAU WAKUBWA SEKTA YA MAZIWA

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina akifungua mkutano wa Jukwaa la Kimataifa la Maziwa uliofanyika jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Serena. Mkutano huo ulishirikisha wadau wakubwa wa sekta ya maziwa kutoka nje na ndani ya nchi. 
Meneja Mwandamizi Biashara ya Kilimo, Huduma ya Ushauri na Utafiti wa Benki ya NMB akizungumza kwenye mkutano wa Jukwaa la Kimataifa la Maziwa uliofanyika jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Serena. 
Baadhi ya viongozi wa Jukwaa la Kimataifa la Maziwa wakiwasilisha mada kwenye mkutano huo ulishirikisha wadau wakubwa wa sekta ya maziwa kutoka nje na ndani ya nchi. 
Baadhi ya viongozi wa Jukwaa la Kimataifa la Maziwa wakiwasilisha mada kwenye mkutano huo ulishirikisha wadau wakubwa wa sekta ya maziwa kutoka nje na ndani ya nchi. 


BENKI ya NMB kwa kushirikiana na Jukwaa la Kimataifa la Maziwa na wadau wengine wameungana kukutanisha wadau wa sekta ya maziwa ili kuangalia namna ya kukuza uzalishaji, uchakataji na matumizi maziwa hususani nchini Tanzania.

Wadau hao zaidi ya 150 kutoka nchi mbalimbali na Tanzania wanakutana kwa siku mbili mfululizo kuangalia namna bora ya kuifanya sekta ya maziwa kufanya vizuri zaidi na kushiriki katika kupunguza umasikini kwa jamii zinazozalisha bidhaa hiyo.

Benki ya NMB imetumia zaidi ya shilingi bilioni 100 kwa ajili ya mikopo kwa wakulima mbalimbali ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali kuinua kilimo ikiwemo sekta ya maziwa nchini.

Kwa upande wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina akizindua mkutano huo leo jijini Dar es Salaam, aliishukuru NMB kwa kukutanisha wadau hao kujadili namna bora ya kuinua sekta hiyo nchini Tanzania.
Baadhi ya wadau wa sekta ya maziwa kutoka nchini Tanzania wakizungumza katika mkutano huo. 
Sehemu ya wadau wakubwa wa sekta ya maziwa kutoka nje na ndani ya nchi wakishiriki katika mkutano huo. 
Sehemu ya wadau wakubwa wa sekta ya maziwa kutoka nje na ndani ya nchi wakishiriki katika mkutano huo. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad