Waziri
wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina akifungua mkutano wa Jukwaa la
Kimataifa la Maziwa uliofanyika jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya
Serena. Mkutano huo ulishirikisha wadau wakubwa wa sekta ya maziwa
kutoka nje na ndani ya nchi.
Meneja
Mwandamizi Biashara ya Kilimo, Huduma ya Ushauri na Utafiti wa Benki ya
NMB akizungumza kwenye mkutano wa Jukwaa la Kimataifa la Maziwa
uliofanyika jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Serena.
Baadhi
ya viongozi wa Jukwaa la Kimataifa la Maziwa wakiwasilisha mada kwenye
mkutano huo ulishirikisha wadau wakubwa wa sekta ya maziwa kutoka nje na
ndani ya nchi.
Baadhi
ya viongozi wa Jukwaa la Kimataifa la Maziwa wakiwasilisha mada kwenye
mkutano huo ulishirikisha wadau wakubwa wa sekta ya maziwa kutoka nje na
ndani ya nchi.
BENKI
ya NMB kwa kushirikiana na Jukwaa la Kimataifa la Maziwa na wadau
wengine wameungana kukutanisha wadau wa sekta ya maziwa ili kuangalia
namna ya kukuza uzalishaji, uchakataji na matumizi maziwa hususani
nchini Tanzania.
Wadau
hao zaidi ya 150 kutoka nchi mbalimbali na Tanzania wanakutana kwa siku
mbili mfululizo kuangalia namna bora ya kuifanya sekta ya maziwa
kufanya vizuri zaidi na kushiriki katika kupunguza umasikini kwa jamii
zinazozalisha bidhaa hiyo.
Benki
ya NMB imetumia zaidi ya shilingi bilioni 100 kwa ajili ya mikopo kwa
wakulima mbalimbali ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali kuinua
kilimo ikiwemo sekta ya maziwa nchini.
Kwa
upande wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina akizindua
mkutano huo leo jijini Dar es Salaam, aliishukuru NMB kwa kukutanisha
wadau hao kujadili namna bora ya kuinua sekta hiyo nchini Tanzania.
Baadhi ya wadau wa sekta ya maziwa kutoka nchini Tanzania wakizungumza katika mkutano huo.
Sehemu ya wadau wakubwa wa sekta ya maziwa kutoka nje na ndani ya nchi wakishiriki katika mkutano huo.
Sehemu ya wadau wakubwa wa sekta ya maziwa kutoka nje na ndani ya nchi wakishiriki katika mkutano huo.
No comments:
Post a Comment