HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, January 25, 2019

WAJUMBE UMOJA WA WABUNGE WANAWAKE TANZANIA WAKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA SHIRIKA LA UMOJA WA KIMATAIFA LA WANAWAKE JIJINI DODOMA

 Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akizungumza na Wajumbe kutoka Umoja wa Wabunge wanawake Tanzania (TWPG) na ugeni kutoka Shirika la Umoja wa kimataifa la wanawake ulioongozwa na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa kimataifa la wanawake Kanda ya Afrika Mashariki na Kati yenye makazi yake Nairobi, Dkt. Izeduwa Derex Briggs kikao kilichofanyika leo tarehe 25 Januari, 2019 katika ofisi za Bunge Jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Wabunge wanawake Tanzania (TWPG), Mhe. Margaret Sitta akiongoza kikao cha pamoja cha Wajumbe kutoka Umoja wa Wabunge wanawake Tanzania (TWPG) na ugeni kutoka Shirika la Umoja wa kimataifa la wanawake  (UN Women) kilichofanyika leo tarehe 25 Januari, 2019 katika ofisi za Bunge Jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa kimataifa la wanawake Kanda ya Afrika Mashariki na Kati yenye makazi yake Nairobi, Dkt. Izeduwa Derex Briggs akizungumza na Wajumbe kutoka Umoja wa Wabunge wanawake Tanzania (hawapo kwenye picha) kikao kilichofanyika leo tarehe 25 Januari, 2019 katika ofisi za Bunge Jijini Dar es Salaam.
 Wajumbe kutoka Umoja wa Wabunge wanawake Tanzania (TWPG) wakiwa katika kikao cha pamoja na ugeni kutoka Shirika la Umoja wa kimataifa la wanawake (UN Women) kilicholenga kufahamiana, kubadilishana uzoefu na kujua shughuli mbali mbali zinazofanywa na Umoja wa Wabunge wanawake Tanzania (TWPG) kikao kilichofanyika leo tarehe 25 Januari, 2019 katika ofisi za Bunge Jijini Dar es Salaam.
Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (wa tatu kulia mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe kutoka Umoja wa Wabunge wanawake Tanzania (TWPG) na ugeni kutoka Shirika la Umoja wa kimataifa la wanawake ulioongozwa na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa kimataifa la wanawake Kanda ya Afrika Mashariki na Kati yenye makazi yake Nairobi, Dkt. Izeduwa Derex Briggs (wanne kulia mbele) kikao kilichofanyika leo tarehe 25 Januari, 2019 katika ofisi za Bunge Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia mbele ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wabunge wanawake Tanzania (TWPG), Mhe. Margaret Sitta na Mjumbe Mhe. Salma Kikwete (wa pili kulia mbele)

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad