HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 10, 2019

NDUGU WASHIRIKI KUFICHA USHAIDI VITENDO VYA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO-SHINYANGA

  Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Watoto kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Sebastian Kitiku akiongea na wadau kujadili hali jumbe zitakazotumika kutokomeza vitendo vya ukatili mkoani Shinyanga leo mjini Shinyanga.
 Afisa Tawala Mkoa wa  Shinyanga Albert Msovela akiongea na wadau kujadili hali jumbe zitakazotumika kutokomeza vitendo vya ukatili mkoani Shinyanga leo mjini Shinyanga.
 Baadhi ya  wadau kujadili hali jumbe zitakazotumika kutokomeza vitendo vya ukatili mkoani Shinyanga leo mjini Shinyanga.
Baadhi ya  Wajumbe  kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii wakiwa Mkoani Shinyanga  kujadili hali jumbe zitakazotumika kutokomeza vitendo vya ukatili.

Na Anthony Ishengoma.
Matendo ya ukatili yaliyolipotiwakatika Jeshi la Polisi hapa Nchini yamefikia 13 elfu mpaka kufikia mwaka jana tofauti na matukio takribani elfu 10 yaliyolipotiwa katika jeshi hilo kwa takwimu za mwaka 2016-17.

Akiongea wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kinachoendelea katika Manispaa ya Shinyanga kujadili jumbe mahususi zitakazotumika katika jitihada za serikali kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoani Shinyanga Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Watoto kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Sebastian Kitiku amesema vitendo vya ukatili vinazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka hapa Nchini.

 Kitiku amewaambia wajumbe wa kikao kazi hicho kuwa Wizara ya Afya inatengeneza jumbe mahususi za kutokomeza ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto na wadau wa Mkoa wa Shinyinga kwa kuwa mkoa wa Shinyanga ni moja ya mikoa inayoongoza katika kiwango kikubwa cha Mimba na Ndoa za utotoni hapa Nchini.

Wakati huohuo Mkurugenzi wa Utawala wa Mkoa wa Shinyanga Albert Msovela amewataka viongozi wa Mkoa na Almashauri, viongozi wa dini, vyombo vya ulinzi na usalama vya Mkoa huo  kuhakikisha wanafanya kazi kubwa kumaliza tatizo hilo kwa kuwa haamini kama tatizo hilo linatokana na mila za wakazi wa mkoa wa Shinyanga.

‘’Siamini kama vitendao hivi vinatoka na mila potofu bali ni mmomonyoko wa maadili kwa kuwa wazazi na walezi wameacha jukumu lao la kuwalea watoto kama inavyostahili bali wanafuata hali ya sasa ya utandawazi’’. Alisema Msovela.

Aidha Msovela alionya kuwa Serikali ya Mkoa wa Shinyanga haitaendelea kuvumilia vitendo hivyo kwa kuwa kwa matukio ya Mkoa huo unaweza ukajiuliza kama unahitaji huruma ya mweneyezi Mungu kwasababu kumekuweko mauaji ya vikongwe, Watu wenye Uaribino, vipigo kwa akina mama na sasa mimba na ndoa za utotoni.

Msovela ametaja takwimu za hali ya ukatili Mkoani humo kuwa ni kubwa kwa kuwa kwasasa mkoa unaonesha una kiasi cha 34% za mimba za utotoni na ndoa za utotoni  ni asilimia ni asilimia 59%na kuzitaka jamii mkoani humo kubadilika ili watoto wa kike wapate fursa ya kutimiza ndoto zao.

Aidha amewaambia wajumbe wa kikao hicho kuwa tatizo la mimba za mapema ni kubwa sana kwani kwa Wilaya ya Kishapu pekee kwa mwaka jana jumla ya watoto 57 wa shule walipata ujauzito.

Ameongeza kuwa kwasasa wazazi wamekuwa wakishirikiana na waalifu kuficha ushaidi baada yukupewa ng’ombe na hivyo kushindwa kutoa taarifa ili waanga wa ukatili waweze kupata haki baada ya kugwa wamefanyiwa vitendao vya ukatili.

‘’Hata ikitokea suala la ukatili limepelekwa mahakamani wanajamii husika wamekuwa hawajitokezi mahakamani kutoa ushahidi jambo ambalo linasababisha utokomezaji wa vitendo vya ukatili kuwa mugumu kwa kuwa mahakama inawaachia huru wahusika kwa kukosa ushaidi’’. Alilamika Kiongozi huyo wa Utawala Mkoani hapo Msovela.

Amemwagiza Afisa Elimu wa Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha walimu wanatoa taarifa za wanafunzi wanaoacha shule kwa sasbabu za ndoa na ujauzito ili mkoa uweze kuchukua zinazostahili ikiwemo kuwafikisha wahusika katika vyombo vya sheria.

Kazi ya kutengeneza ujumbe kwa ajili ya kutokomeza mimba na ndoa za utotoni inaendelea itaendelea katika mikoa yenye takwimu za juu katika ukatili dhidi ya wanawake na watoto ambayo ni mikoa ya Shinyanga, Tabora, Singida na Rukwa.   

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad