HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 3, 2019

DC MUHEZA:NITASHIRIKIANA NA WANAMICHEZO KUHAKIKISHA TUNAPATA TIMU YA LIGI KUU

MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati akifunga Mashindano ya Kombe la Kabunda Cup
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akimkabidhi Kombe la Ubingwa wa Mashindano ya Kabunda Cup Nahodha wa timu ya Ushirika Amiri Nko kushoto ni Afisa Michezo wa wilaya ya Muheza Anania Sama
 Nahodha wa timu ya Ushirika Amiri Nkoa akiwa ameinua kombe hilo juu mara baada ya kukabidhiwa.
MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akimkabidhi Kitita cha Milioni moja Nahodha wa timu ya Ushirika Amiri Nko baada ya timu yao kuibuka na ushindi kwenye michuano ya Kombe la Kabunda Cup kushoto ni Afisa Michezo wa wilaya ya Muheza Anania Sama
 Katibu Msaidizi wa Kamati ya Mashindano hayo akisoma risala
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo katika akiwa kwenye picha ya pamoja na wachezaji
 Sehemu ya Mashabiki wa soka wakiwa wamnefuatilia mchezo huo


MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Mwanasha Tumbo amesema atashirikiana na wanamichezo ili kuhakikisha wanaweza mazingira mazuri yatakayowezesha kupatikana timu ambayo itaweza kushiriki ligi madaraja ya juu ikiwemo Ligi kuu.

Mwanasha aliyasema hayo wakati fainali michuano ya kombe la Kabunda Cup iliyokuwa ikichezwa kwenye viwanja vya Vikonge Mtindiro wilayani Muheza ambapo alisema ili kuweza kuhakikisha wanafanikisha jambo hilo wataendelea kuhamasisha vijana kujikita kwenye michezo.

Alisema licha ya kuhamasisha michezo kutokana na kwamba ni ajira ambayo inaweza kuwainua vijana kuichumi na kupata maendeleo lakini pia aliwahaidi kuwajengea kiwanja cha mpira chenye matofali ili waweze kuonyesha umahiri wao na hatimaye wilaya hiyo iweze kupata mafanikio kwenye soka.

“Leo nimekuja hapa kuhimitisha Ligi hii kwanza nimefurahishwa sana na viwango ambavyo mmekuwa mkivionyesha kwenye mchezo huu nimeongeza na Diwani wenu hapa na niwahaidi kwamba nitawajengea kiwanja chenye matofali ili hari ya kushiriki kwenye michezo muweza kuendelea nayo na tunaamini siku zijazo tutairudisha Muheza kwenye ramani ya soka “Alisema DC Mwanasha.

Alisema kwamba anafanya hivyo ili kuweza kuchochea maendeleo ya mchezo huo ambao vijana wakiweka bidii na nia wanaweza kufika mbali ikiwemo kuitangaza wilaya hiyo lakini pia kupata manufaa kama walivyokuwa Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu ambao wanacheza soka la kulipwa nje ya nchi.

Awali akizungumza katika fainali hiyo Katibu Msaidizi wa Kamati ya Mashindano hayo Salehe Mwinjuma alisema lengo la mashindano hayo yalikuwa ni kuweza kuinua vipaji vya wachezaji wachanga kwenye Kata hiyo yaliyoanzishwa na mdau wa michezo Seif Kabunda kwa kushirikisha timu 20 zilizocheza kwa mtindo wa makundi.

Alisema kwamba msimu ujao ligi hiyo itakuwa na mabadiliko makubwa kutokana na mdhamini wa mashindano hayo kuamua kujipanga upya na kuja kinyengine lengo kubwa likiwa kuhakikisha michezo inapata mafanikio.

Katika fainali hiyo timu ya Ushirika FC waliweza kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 na kutawazwa kuwa mabingwa wapya wa Kombe la Kabunda Cup baada ya kuibamiza Kwarabuye FC mabao 2-1 katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Vikonge Mtindiro na kujiny’akulia kombe na kitita cha sh.milioni moja . Katika mchezo huo ambao ulikuwa mkali na wenye ushindani mkubwa uliohudhuriwa na Mkuu wa wilaya ya Muheza Mwanasha Tumbo ambaye ndie alikabidhi zawadi kwa washindi kwenye michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad