HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, December 15, 2018

Mhagama:Taasisi za serikali na binafsi zatakiwa kujisajili OSHA

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
SERIKALI imeagiza amezitaka taasisi zote za na binafsi kuhakikisha  wanajisajili kupitia   Wakala Afya, Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) ili kutekeleza matakwa ya sheria. Hayo ameyasema Waziri  wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi Vijana na Ajira Jenista Mhagama alipowatembelea na kuzungumza na wafanyakazi wa OSHA na kuangalia utendaji wao wa kazi katika kusimamia masuala aya usalama mahala pa kazi

Amesema uwepo wa taasisi ya OSHA ni muhimu kwa kuwa inalenga  kuondoa dosari za aina mbalimbali hususani  madhara  katika maeneo ya kazi ambapo bila kufanya hivyo wafanyakazi wangekuwa waadhirika wakubwa katika sehemu za kazi zao.

“Taasisi zote na kampuni kujisajili na OSHA ili ziweze kufanya kazi kwa utaratibu wa kisheria, hii aina maana ina faida kwa Serikali, bali ni  faida kwa   taasisi , wafanyakazi wote kwa kuwa zaidi imelenga kuhakikisha inaondoa mazingira yote hatarishi ambayo pengine yangeweza kuleta madhara mahala Pa kazi ” amesema Mhagama.

 Waziri Mhagama amaesema tangu kuanzishwa kwa chombo hicho  kumekuwa na  maendeleo  ya usalama na afya za wafanyakazi yameweza kuonekana ambapo alisisitiza kuwa ili kufikia malengo ya kuanzishwa kwa Wakala  huyo ni  taasisi zote hazina budi kuhakikisha zinajisajili.

Amesema katika kuhakikisha OSHA inafanya kazi zake kwa weledi na kuziwezesha taasisi mbalimbali kujisajili, tozo mbalimbali zilizokuwa zikitozwa kwa ajili ya usajili zimeondolewa, lengo likiwa kuzipunguzia mzigo taasisi hizo na kuzifanya zijisajili na wakala huyo kama ambavyo sheria ya Wakala wa Serikali Namba 30 ya Mwaka 1997 imeagiza.

Aidha aliitaka OSHA kuzidi kujihimarisha kiutendaji huku akiahidi kuwa Serikali itaendelea kuitazama kwa jicho la karibu ili iweze kutimiza malengo yake ya utendaji kawa weledi na kuamini kuwa kama wakala huyo akiwezeshwa ataweza kufanya kazi zake kwa weledi.

Mhagama amezipongeza  alizipongeza taasisi mbalimbali za Umma zinazoendelea kuitikia wito wa sheria hiyo kwa kujisajili na Wakala huyo, akisisitiza kuwa kwa kufanya hivyo kutasaidia kuondoa magonjwa, ajali na kuweka mazingira mazuri ya utendaji kwa taasisi hizo na hivyo kuongeza tija katika utendaji wa kazi.

Kwa upande wake Kaimu  Mtendaji Mkuu wa OSHA Hajida Mwenda, mbali na kuainisha majukumu mbalimbali yanayotekelezwa na wakala huyo, alisema tangu kuanzishwa kwake OSHA imezidi kupiga hatua na kufanikisha kuondoa vikwazo vilivyokuwemo katika utendaji wa taasisi mbalimbali.

Amesema katika kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake,OSHA imezidi kupiga hatua mbalimbali na kufanikiwa kutoa  elimu ya  uelewa kwa wananchi, hatua iliyowezesha kuongeza wigo wa taasisi hizo kujisajili.
Waziri  wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi Vijana na Ajira Jenista Mhagama akizungumza na wafanyakazi wa Dawasa walioko katika mafunzo ya Ukimwi yanayoendeshwa  na Wakala Afya, Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) wakati alipotembela ofisi za OSHA jijini Dar es Salaam.
Kaimu  Mtendaji Mkuu wa OSHA Hajida Mwenda akizungumza na waandishi habari kuhusiana na usimamizi wafanyakazi mahala pa kazi katika utoaji wa elimu wakati Waziri  wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi Vijana na Ajira Jenista Mhagama alipotembelea ofisi za OSHA jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wafanyakazi wa Dawasa wakiwa katika mafunzo ya UKIMWI yanayoendeshwa na OSHA jijini Dar es Salaam.

afanyakazi wakiwa katika mkutano na Waziri  wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi Vijana na Ajira Jenista Mhagama alipotembelea ofisi za OSHA jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad