HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 31, 2018

MABONDIA WAPIMA UZITO KUZIPIGA DESEMBA 31 UWANJA WA KINESI

Mabondia Azizi Uliza na Ramadhani Shauri wamepima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa Desema 31, 2018 mpambano wa kufunga mwaka na kufungua mwaka. Aliyekuwa wa kwanza kabisa kuingia katika viwanja vya las Vegasi Mabibo kwa ajili ya kupima uzito ni Azizi Uliza aliyeingia uwanjani kwa shangwe na ndelomo uku akisindikizwa na wapambe wake pamoja na vigoma.

Baara ya Saa moja Bondia Ramadhani Shauri naye akaingia na shangwe na ndelemo, vifijo zaidi ya mwenzake hata hivyo nani zaidi ya mwenzie itajulikana katika uwanja wa Kinesi, Shekilango jijini Dar es Salaam ambapo pambano hilo litapigwa kwa Raundi 10.

Akizungumzia mpambano huo, Promota  Josepher Nyilawila kutoka Kampuni ya Ijuka Sports amesema kuwa ulizi utakuwa ni wa kutosha, amesema mbali na mpambano uho siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine yatakayowakutanisha mabondia mbalimbali ambapo Hussein Itaba atazipiga na Kanda Kabongo na Tonny Rashidi atazichapa na Nassoro Madimba kutoka Bagamoyo maeneo ya Kiwangwa na Rolen Japhert atazikunja na Mohamedi Kashinde 'Simba wa Mbagala' naye Baina Mazola ataoneshana umwamba na Faraji Sayuni.

Amesema mapambano yote hayo yatakuwa kwa kingilio cha Tsh 6000 na kwa V.I.P 10, 000 ambapo utashuhudia mapambano yote
Bondia Mussa Msabaha kushoto akitunishiana misuli na Ibrahimu Makubi baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa kufunga mwaka utakaofanyika Desemba 31 katika viwanja vya Kinesi Shekilango maeneo ya Urafiki Picha na Super D Boxing News
Bondia Azizi Uliza akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake wa kufunga mwaka utakaofanyika Desemba 31 katika uwanja wa kinesi uliopo Shekilango akizipiga na Ramadhani Shauri mpambano wa Raundi kumi.
Wasichana wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa kufunga mwaka utakaofanyika Desemba 31 katika viwanja vya Kinesi Shekilango maeneo ya Urafiki

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad