HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 31, 2018

IGP SIRRO AZINDUA RASMI CHAMA CHA WASTAAFU WA JESHI LA POLISI (TARPOA)

Mwenyekiti wa Chama cha Wastaafu wa Jeshi la Polisi (TARPOA) Kamishna Mstaafu CP Suleiman Kova (Kushoto), akimkabidhi zawadi Kamishna wa Kamisheni ya Ushirikishwaji wa Jamii Mussa Ali Mussa kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, katika sherehe za Uzinduzi Rasmi wa chama hicho zilizofanyika mwishoni mwa juma katika bwalo la maafisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es salaam. Picha na Jeshi la Polisi.
Mgeni Rasmi Kamishna wa Kamisheni ya Ushirikishwaji wa Jamii CP Mussa Ali Mussa kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, akiwaongoza aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu IGP Said A. Mwema (kulia) na kamishna mstaafu suleiman Kova ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Wastaafu wa Jeshi la Polisi (TARPOA) katika zoezi la kukata utepe wakati wa sherehe za Uzinduzi Rasmi wa Chama hicho zilizofanyika mwishoni mwa juma katika bwalo la maafisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es salaam. Picha na Jeshi la Polisi.
Baadhi ya Wastaafu wa Jeshi la Polisi ambao pia ni Wanachama wa Chama cha Wastaafu wa Jeshi hilo TARPOA wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea wakati wa sherehe za Uzinduzi Rasmi wa Chama hicho kilichoanzishwa mwaka 2006 na aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Mstaafu Said Mwema. Picha na Jeshi la Polisi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad