HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 7, 2018

UINGEREZA KUSAIDIA JUHUDI ZA TANZANIA KUONGEZA IDADI YA WATALII KUPITIA ATCL.

Na Geofrey Tengeneza

Mwakilishi wa Serikali ya Uingereza katika masuala ya biashara  Andrew Rosindell 

ameahidi kusaidia kufanikisha mpango wa Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) kufanya

Safari zake London, Uingereza.

 Rosindelli alitoa ahadi hiyo jana alipokutana na kuwa na mzungumzo na Naibu 

Katibu Mkuu wa WIzara ya Maliasili na Utalii Dkt Aloyce Nzuki katika maonesho ya utalii ya 

World Travel Market yanayoendelea jijini London Uingereza ambapo alimuomba mwakilishi 

huyo kusaidia mpango huo ambao alisema utasaidia sana kuongeza idadi ya watalii 

wanaotembelea Tanzania kutoka Uingereza.


Aidha Dkt.Nzuki amemuomba Rosindell kuandaa mkutano wa pamoja baina yawafanyabiashara wa Tanzania na Uingereza mapema iwezekanavyo ili kujadiliana namna ya 

kuimarisha ushirikiano wa kibiashara baina ya wafanyabiashara wa Tanzania na Uingereza kwa

manufaa ya nchi hizo mbili.






Aidha, Dkt.Nzuki ameweza kukutana na kufanya mazungunzo na Mjumbe maalum ambaye pia 

ni Mbunge wa nchi hiyo Andrew Rosindell ambaye ni mbunge aliteuliwa na Waziri Mkuu huyo 

kuwa Mwakilishi wa Serikali ya Uingereza wa masuala ya Biashara (Trade Envoy) ambaye 

miongoni mwa kazi zake ni kukuza biashara, uwekezaji na Utalii baina ya Uingereza na 

Tanzania.


Katika hatua nyingine Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Dkt.Hamisi Kigwangalla 

amepongeza timu ya Tanzania inayoshiriki maonyesho hayo kwa kazi nzuri ya kuitangaza 

vyema Tanzania kama eneo bora la utalii Afrika na Duniani kwa ujumla.


Kupitia ukurasa wake Twitter aliandika "hii ni taswira ya leo ya banda letu la maonesho kule

jijini London, kwenye World Travel Market (WTM), Uingereza, ambapo slogan yetu ya 

Tanzania Unforgettable! imetumika ipasavyo kuuza vivutio vyetu. Nawapongeza sana washiriki

wote kutoka Tanzania na wa Kamati yetu ya Destination Branding chini ya uenyekiti wa  

Devotha Mdachi kwa kazi nzuri. Huu ni mwanzo tu” aliandika DKt Kingwangala. 


Ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo umeratibiwa na Bodi ya Utalii Tanzania –TTB 
ambapo timu ya washiriki kutoka Tanzania ikijumuisha waoneshaji kutoka sekta ya umma na

binafsi inaongozwa inaongozwa na Naibu Katibu MKuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt.

Aloyce Nzuki.

Naibu Katibu Mkuu Maliasili na Utalii, Dkt.Aloyce Nzuki akimkabidhi majarida na vipeperushi vya utalii wa Tanzania (promotional materials) mwakilishi wa Serikali ya Uingereza katika masuala ya biashara  Andrew Rosindell .


Mwakilishi wa Serikali ya Uingereza katika masuala ya biashara  Andrew Rosindell  akisoma moja ya majarida ya utalii alipotembelea banda la 
Tanzannia katika maonesho ya World Travel Market jijini London Uingereza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad