HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 9, 2018

PWANI YAKAMATA LUNINGA KUMI ZA WIZI,WEZI TISA AKIWEMO WA MAFUTA KWENYE MRADI WA UJENZI WA STANDARD GAUGE-WANKYO


Na Mwamvua Mwinyi, Pwani 
JESHI la polisi mkoani Pwani, limekamata luninga kumi flat screen zenye thamani ya sh. mil.18, ambazo ziliibiwa katika matukio mbalimbali ya uvunjaji, mkoani humo. 

Aidha linamshikilia mtu mmoja jina limehifadhiwa baada ya kukutwa akiwa na madumu kumi yenye ujazo wa lita 20 ya mafuta aina ya dizeli  ,aliyoiba katika mradi wa ujenzi wa reli ya standard gauge , Soga wilaya ya kipolisi Mlandizi. 

Akithibitisha kutokea kwa matukio hayo, kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP)  Wankyo Nyigesa alisema, wanashikilia watu nane kwa tuhuma za kuhusika kwenye matukio hayo. 

Nyigesa alieleza katika msako huo wamekamata jenereta mbili kubwa zenye thamani ya milioni 6.5 ambazo ni aina ya Euro power EP. 6500E na boss BG -2500 .

Alifafanua, vitu vingine vilivyokamatwa ni deki mbili, vingamuzi viwili, speaker mbili, music system mbili, home fieta moja, rimoti sita, speaker twiter mbili, flash moja kapeti za chini ya sakafu mbili, stendi ya vyombo moja na extention moja. 

Hata hivyo kamanda huyo alisema , mtuhumiwa aliyekamatwa kijiji cha Mperamumbi akiwa amepakia mafuta kwenye pikipiki aina ya sanlg namba MC. 197 BJD kutoka mradi wa standard gauge wanamhoji na atafikishwa mahakamani. 

Katika tukio jingine wamekamata pikipiki saba na bangi kiroba kimoja kilichokuwa kinasafirishwa kwenda kuuzwa. 

Nyigesa alibainisha, katika tukio hilo mmiliki wa pikipiki yenye namba za usajili MC 951 BSA  anaombwa kujisalimisha mwenyewe kituo chochote cha polisi ndani ya siku tatu vinginevyo watamsaka popote ili kueleza kuhusu bangi hiyo.  

"Sisi wakati tukiwa kwenye hapa kazi tuu, wao wapo kwenye wizi tuu, tunawapa salamu wakati wengine wakifyekelea mbali, kwa sisi mkoa wa Pwani tunaendelea na operesheni na msako wa TINDUA TINDUA, tutatindua mpaka kieleweke "alisisitiza Nyigesa. 

Alitoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kununua vitu mikononi bila ya kupewa risiti kwani atakaekutwa na mali ya wizi nae atachukuliwa hatua za kisheria. 

Nyigesa aliwaasa pia kuwa ,wabia katika suala la ulinzi shirikishi kwenye maeneo yao ili kukabiliana na ujambazi, uvunjaji na uhalifu mbalimbali.
Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP)  Wankyo Nyigesa akionyesha baadhi ya luninga flat screen zilizoibiwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo (picha na Mwamvua Mwinyi)

Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP)  Wankyo Nyigesa akielezea msako endelevu unaendelea mkoa humo huku akieleza kauli mbiu yake ya Tindua Tindua hadi kieleweke. (picha na Mwamvua Mwinyi)

Mmoja wa watu walioibiwa luninga zao, mzee Lebul Mfinanga (wa kulia aliyebeba luninga) akiwa ametoka kutambua luninga yake makao makuu ya polisi Pwani . (picha na Mwamvua Mwinyi) 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad