HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 5, 2018

MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA CRDB AMTEMEBELA GAVANA WA BENKI KUU

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florence Luoga (katikati) akiwa katika mazungumzo na viongozi wa Benki ya CRDB, waliofika ofisini kwake mwishoni mwa wiki kwa lengo la kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji mpya, Abdulmajid Nsekela (kulia) aliyeambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Ally Laay (wa pili kulia) wengine pichani ni Manaibu Gavana, Dkt. Bernard Kibesse (kushoto) na Dkt. Julian Banzi.
Manaibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernard Kibesse (wa pili kushoto) na Dkt. Julian Banzi (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kulia) aliyeambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Ally Laay (kulia), baada ya kikao chao, kilichofanyika kwenye ofisi ya Gavana wa Benki Kuu, jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
Manaibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernard Kibesse (wa tano kushoto) na Dkt. Julian Banzi (wa nne kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa tano kulia) pamoja na ujumbe wa Benki hiyo.
Baadhi ya viongozi wa Benki ya CRDB wakipatiwa maelezo walipokuwa wakiangalia picha za Gavana mbalimbali waliopita.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad