HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 29, 2018

MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA CRDB AKUTANA NA NAIBU WAZIRI SHONZA, ATEMBELEA NHC

Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakati akizungumzia mikakati mbalimbali ya kibenki pamoja na ushirikiano wa kibiashara kati ya Benki hiyo na Serikali, kikao kilichofanyika kwenye makao makuu ya Benki ya CRDB, Azikiwe jijini Dar es salaam hivi karibuni.
Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akisaini kitabu cha wageni wakati alipomtembelea Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, ofisini kwake, Azikiwe jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Maulidi Banyani alipomtemebela ofisini kwake, jijini Dar es salaam leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kulia), akifurahi jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Maulidi Banyani (katikati) wakati kikao chao kilichofanyika leo, jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dorah Ngaliga (kulia), Mkurugenzi wa Utawala wa Benki hiyo, Beatus Segeja (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Muendelezaji Biashara wa NHC, William Genya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza jambo katika kikao kilichokutanisha uongozi wa Benki hiyo na Shirika la Nyumba nchini (NHC), kilichofanyika kwenye makao makuu ya NHC, jijini Dar es salaam leo. Wengine pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dk. Maulidi Banyani pamoja na Manaibu Wakurugenzi Wakuu wa Benki ya CRDB, Dorah Ngaliga (kulia) na Esther Kitoka.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad