HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, November 24, 2018

Dkt. Mwakyembe azindua Kampeni ya Uzalendo na Utaifa 2018, yenya kauli mbiu “Kiswahili uhai wetu,Utashi wetu”

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akisisitiza jambo  kwa wadau wa Wizara hiyo katika  hafla fupi  ya Uzinduzi wa Uzalendo na Utaifa iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam .
 Kaimu Mkurungezi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa  Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Leah Kihimbi akiongea jambo na wadau wa Wizara hiyo (Hawapo katika picha) katika  hafla fupi ya Uzinduzi wa  Kampeni ya Uzalendo na Utaifa leo Jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mawasiliano na Uhusinao wa Umma kutoka benki ya NBC Bw. William Kallage ambao  ndio Wadhamini Wakuu wa Kampeni ya Uzalendo na Utaifa mwaka  huu inayotarajiwa kufanyika tarehe 8  Disemba  2018 Jijini Dodoma, akieleza jambo kwa wadau wenzake waliofika kuunga mkono uzinduzi wa kampeni hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurungezi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa,  Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Leah Kihimbi(kulia) akimvalisha nembo inayoashiria uzalendo Mkuu wa Mawasiliano na Uhusinao wa Umma kutoka benki ya NBC Bw. William Kallage ambao ndio wadhamini wakuu wa Kampeni ya Uzalendo na Utaifa mwaka  huu inayotarajiwa kufanyika tarehe 8  Disemba  jijini Dodoma.
 Wadau wa Sanaa kutoka katika sekta binafsi taasisi za Serikali wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea  katika  hafla fupi ya uzinduzi wa Kampeni ya Uzalendo na Utaifa leo Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad