HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 30, 2018

Dkt. Mahiga akutana na Viongozi kutoka Norway, Denmark, Venezuela na China

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga wa pili kutoka kushoto ukiwa katika mazungumzo na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam leo. Viongozi hao walijadili namna ya kukuza na kuimarisha ushirikiano hususan wa kibiashara ikiwemo mchakato wa kampuni ya Equinor wa kuzalisha gesi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kusafirisha nje ya nchi. 
Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup wa pili kutoka kulia akisisitiza jambo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga wa pili kutoka kushoto akiongea wakati wa mkutano wake na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup. Wengine katika picha kutoka kulia ni Katibu wa Mhe. Waziri, Bw. Magabilo Murobi, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Jestas Nyamanga na Afisa Dawati, Bi. Tunsume Mwangolombe
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiagana na mgeni wake, Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup baada ya kufanya mazunguzmo ambayo yalikuwa ya mafanikio makubwa katika mustakabali wa Tanzania na Norway. 
Picha ya pamoja.
Mazungumzo na Mhe. Zhui Yuxiao, Balozi anayesimamia masuala ya Jukwaa la Ushirikiano wa China na Afrika (FOCAC) 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga amekutana na Balozi Zhui Yuxiao, Mwakilishi kutoka China anayesimamia masuala ya Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Wawili hao walijadili utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa FOCAC uliofanyika Beijing mwezi Agosti 2018. Wamekubaliana kuundwa kwa kamati ya utekelezaji ambayo itaratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje ambapo Wizara imetakiwa pia kuteua mtumishi mmoja mwandamizi awe mratibu wa masuala ya FOCAC. 
Balozi Zhui Yuxiao, Mwakilishi kutoka China anayesimamia masuala ya Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga. Mwingine ni Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Wang Ke. 
Picha ya pamoja.

Mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga katikati akiwa katika mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura hayupo pichani. Wengine ni Katibu wa Mhe. Waziri, Bw. Magabilo Murobi na Afisa Dawati, Bi. Lillian Kimaro. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura katikati akiwa katika mazungumzo na mwenyeji wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga. Mhe. Naibu Waziri pamoja na mambo mengine ameleta ujumbe kuwa Venezuela inataka kufungua ofisi ya ubalozi nchini jambo ambalo Mhe. Mahiga amelikaribisha kwa mikono miwili na kueleza kuwa endapo Venezuela itafungua ubalozi itakuwa nchi ya nne kutoka Latin Amerika kuwa na ofisi ya Ubalozi Tanzania.
Ujumbe wa Venezuela wa kuomba kufungua ubalozi nchini. 
Picha ya pamoja 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiagana na mgeni wake, AdNaibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura 
Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga wa pili kutoka kushoto ukiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen. Katibu Mkuu alikuja kupata ufafanuzi kuhusu masuala ya haki za binadamu na kuihakikishia Tanzania kuwa haijasitisha msaada wake kwa Tanzania. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiongea wakati wa mkutano wake na Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen. Wengine katika picha kutoka kulia ni Katibu wa Mhe. Waziri, Bw. Magabilo Murobi na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Jestas Nyamanga.
Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen wa kwanza kulia akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiagana na mgeni wake, Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen 

Mkutano na Waandishi wa Habari
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga baada ya kumaliza mazungumzo na wageni wake aliongea na waandishi wa habari ili kupitia kwao wananchi waweze kujua masuala yaliyojadiliwa kwa ajili ya manufaa ya nchi yao. 
Baadhi ya wanahabari waliohudhuria mkutano na Mhe. Waziri. 
Sehemu nyingine ya wanahabari. 
Mkutano unaendelea 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad