HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 15, 2018

CGP KASIKE AFANYA ZIARA GEREZA LA WILAYA MAKETE, MKOANI JOMBE

  Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini (CGP) Phaustine Kasike akiwasili Gereza Makete tayari kwa ziara yake ya kikazi Mkoani Njombe, Novemba 14,  2018.
 Mkuu wa Gereza Makete, SP. Aloyce Kayera(kushoto) akisoma taarifa ya Gereza mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini (CGP) Phaustine Kasike(kulia) alipotembelea gereza hilo leo Novemba 14, 2018.
 Mkuu wa Jeshi la Magereza Nchini (CGP) Phaustine Kasike akizungumza jambo alipotembelea Ofisi za Mkuu wa Wilaya Makete Novemba 14, 2018. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo.
 Baadhi ya Askari wa kike wa Jeshi la Magereza wakiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike ambapo askari hao wamempongeza Mkuu wa Jeshi hilo kwa uamuzi wake wa kutembelea magereza mbalimbali hapa nchini.
 Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akikagua maandalizi ya mashamba ya kilimo cha mahindi katika eneo la Gereza Ludewa mapema leo asbuhi Novemba 14, 2018  kabla ya kuelekea Gereza Makete kuendelea na ziara yake ya kikazi.
Mkuu wa Wilaya ya Makete, Mhe. Veronica Kessy akiagana na Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike alipotembelea Ofisi za Mkuu wa Wilaya Makete.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad