HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 15, 2018

BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAWAFUNDA WANACHAMA WAKE KUHUSU UONGOZI NA UTAWALA BORA

 Mkufunzi kutoka Baraza la Kilimo Tanzania Dkt Freddy Gamba akisisitiza jambo wakati akitoa mafunzo ya Uongozi na Utawala bora kwa wanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania, ambapo wanachama hao wanatarajia kunufaika na mafunzo hayo kwa siku mbili yanayofanyika Dar es Salaam, huku lengo kuu ikiwa ni kuwajengea uwezo kiutendaji wanachama wa baraza katika taasisi wanazoziongoza. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Tanzania Bi Janeth Bitegeko akisisitiza jambo kwa wanachama wa Baraza la Kilimo wanaoshiriki semina ya siku mbili ya Uongozi na Utawala bora, mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo zaidi wa kiutendaji wanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania ambao ni viongozi katika taasisi wanazoziongoza.
 Afisa Sera kutoka Baraza la Kilimo Tanzania Bi Neema Nyamubi na baadhi ya wanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania wakifuatilia kwa makini mafunzo ya Uongozi na Utawala bora, mafunzo hayo ya siku mbili yanayofanyika Dar es Salaam yanaratibiwa na Baraza la Kilimo Tanzania.
 Baadhi ya wanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania ambao wanatoka kwenye Taasisi za TAMPRODA, SECO,  SUWA Farmers Association, Agri link Tanzania na Morogoro Rural Agro Dealers  Association, wakifuatilia mafunzo ya Uongozi na Utawala bora, mafunzo hayo ya siku mbili yanayofanyika Dar es Salaam yameratibiwa na Baraza la Kilimo Tanzania.
 Mwenyekiti wa taasisi ya Morogoro Rural Agro Bw Michael Mpembwa akijadili jambo na washiriki wenzake na wa semina ya uongozi na uatawala bora, mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wa kiutendaji wanachama wa baraza la kilimo Tanzania.
Afisa Uhamasishaji Maendeleo ya wanachama na Uhusiano Kimtandao kutoka Baraza la Kilimo Tanzania Bw Khalid Ngasa na washiriki wengine wa semina ya siku mbili ya Uongozi na Utawala Bora, Semina hiyo imelenga katika kuwajengea uwezo zaidi wa kiutendaji wa wanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania ambao ni viongozi katika taasisi wanazoziongoza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad