HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 17, 2018

SERIKALI IMEZITAKA HALMASHAURI KUWA NA ONE STOP CENTRES KUPAMBANA NA VITENDO VYA UKATILI NCHINI

Na Mwandishi wetu Pwani
Serikali imezitaka Halmashauri  zote Nchini kuhakikisha zinakuwa na vituo vya huduma za  mkono kwa mkono (Ones Stop Centre) ili kuunga mkono serikali katika juhudi zake za kupambana na vitendo vya ukatili hapa Nchini.

Hayo yamesema leo wilayani kibaha mkoani Pwani Naibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipotembelea kituo cha huduma za mkono kwa mkono kilichopo katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani iliyoko Kibaha mkoani humo. 

Dkt. Ndugulile amesema kuwa lengo la vituo hivyo linalenga kupunguza mlolongo wa huduma kwa muhanga wa ukatili kwani vituo hivyo vinatoa huduma za matibabu, huduma za polisi na ushahuri wa kisaikolojia kutoka kwa Afisa Ustawi wa Jamii kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.

Aidha Dkt. Ndugulile amesema nchi kwa sasa ina vituo vikumi tu hivyo kutaka maeneo Mikoa mingine kuiga Mkoa wa Pwani kuhunga mkono juhudi hizi kwa kuwa takwimu zilizopo zinaonesha Tanzania ina ina matukio ya ukatili 41,000 na kati ya matukio hayo 13,000 ni ukatili dhidi ya watoto akitaja hali hiyo kuwa ni ujambazi mpya zidi ya binadamu.

Amezitaja juhudi nyingine za kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto kuwa ni kuwepo kwa madawati ya Jinsia katika vituo vya polisi akitaja idadi ya vituo hivyo kote Nchini kuwa ni jumla ya madawati 500.

Ameongeza kuwa Serikali inawajengea uwezomwalimu wa Shule za Msingi na Sekondari ili kuwa na madawati ya ukatili wa kijinsia kwani vitendo vingi vya ukatili kwa watoto vinatokea katika eneo la shule.

Dkt. Ndugulile pia ameitaka jamii kutofumbia macho vitendo vya ukatili vinavyotokea katika maeneo yao hasa nyumbana katika familia na amesema Serikali itawachukulia hatua watoa huduma za fya watakaojihushisha na uitoaji wa taarifa za uongo kuhusu mashauri ya vitendo vya ukatili.

‘’Baadhi ya wanajamii hapa nchini wanafurahia vitendo vya ukatili kwani wamekuwa wakimalizana kifamilia na kusababisha vitendo hivi kuendelea” alisisitiza Dkt. Ndugulile.

Naibu Waziri Ndugulile ameuagiza Mkoa wa Pwani pamoja na mikoa mingine Nchini kuanzisha dawati la ulinzi wa wanawake na watoto akiongeza kuwa ili ni agizo la serikali hivyo ni lazima mikoa yote Nchini inakuwa na madawati haya ili kutekeleza agizo la serikali.

Akiongea na watumishi wa hospitali ya Tumbi Dkt. Ndugulile amesema kumekuwepo  na kasumba ya adaktari ya kuficha ushahidi kwa watu waliofanyiwa vitendo vya ukatili na kuongeza kuwa hilo ni kosa kisheria na atakayebainika kuficha ushaidi adhabu yake ni kufutiwa usajili.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile yupo katika ziara yake ya siku mbili katika mikoa ya Pwani anmbapo anatembelea na kukagua huduma za afya na maendeleo ya jamii.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Engineer Evalist Ndikilo  kuhusu masuala Afya pamoja na Maendeleo ya Jamii mapema leo ofisini kwake Kibaha Mkoani Pwani.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile pamoja na Mkurugezi Mkuu wa hospitali ya Tumbi Dkt. Edward Wayi akitoa maelezo ya Kituo cha Mkono kwa Mkono (one stop centre) kwa waandishi wa habali kuhusu masuala ya ukatili wa kijinsia mapema leo Tumbi Kibaha Mkoani Pwani.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile pamoja na Mkurugezi Mkuu wa hospitali ya Tumbi Dkt. Edward Wayi akiongea na wagonjwa alipotembelea na kufanya ukaguzi wa hospitali ya rufaa ya Tumbi Kibaha Mkoani Pwani. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad