HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 19, 2018

RAIS MAGUFULI ATOA MILION 50 KWA TAIFA STARS

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametoa kiasi cha Milioni 50 kwa timu ya Taifa ya Tanzania.

Fedha hizo ni  kwa ajili ya safari ya mchezo wa marudiano baina ya Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' dhidi ya Lesotho utakaochezwa Novemba 16.

Akiwa anazungumza na wachezaji na viongozi katika hafla ya chakula cha Mchana Ikulu Jijini Dar es Salaam, Dkt Magufuli amesema kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya safari na sio kwa wasindikizaji.

“Nawapa Millioni 50 kwa ajili ya safari ya Lesotho, fedha hizi zitumike kwa ajili ya wanaotakiwa kusafiri tu, sio mambo ya wachezaji 15, viongozi wasindikazaji 30. Haya mambo yafikie mwisho.” amesema Dkt Magufuli.

Mbali na hilo amewataka wachezaji kujituma na kuacha mambo ya kihuni, "Wachezaji wasipoacha uhuni watakuwa wanafunga magoli mengine ila ya uwanjani watashindwa"

Taifa Stars  katika mchezo uliopita dhidi ya Cape Verde walifanikiwa kuondoka na ushindi wa goli 2-0 mechi iliyopigwa kwenye dimba la Uwanja wa Taifa na kufikisha jumla ya alama 5 akishika nafasi ya pili nyuma ya Uganda.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad