HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 11, 2018

BENKI YA TIB CORPORATE WAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUWATEMBELEA TRC, NIC

BENKI ya TIB Corporate washeherekea wiki ya huduma kwa wateja kwa kutembelea wateja wake.

Leo Oktoba 11 benki hiyo wamewatembelea Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Shirika la Bima la Taifa (NIC) ikiwa ni kwaajili ya kuwashukuru pamoja na kujitadhimini jinsi ya utoaji wa huduma kwa wateja wao.

Akizungumza na wafanyakazi wa benki hiyo Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa amewashukuru wafanyakazi wa benki hiyo kwa kuwaona wamhimu katika kuendeleza gurudumu serikali ya viwanda hapa nchini kwa utunzaji wa fedha.

Nae Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga amewashukuru kwa kuona nchango wa shirika hilo pia pia amewaasa kujitangaza zaidi ili kuondoa mkanganyiko uliopo katika jina la benki hiyo.
Wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate wakimkabidhi ua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa baada ya kutembelewa ofisini kwake na wafanyakazi wa TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru wateja wa benki hiyo katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja.


Mkurugenzi mkuu wa benki ya TIB Corporate Frank Nyabundege akizungumza na wafanyakazi wa beki ya TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka ifikapo Oktoba.
 Mfanyakazi wa benki ya TIB Corporate  akizungumza na wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate hawapo pichani jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja.


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa  akifurahia jambo mara baada ya kutembelewa na wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo.
Wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate na mfanyakazi wa malaka ya reli Tanzania wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa hayupo pichani mara walikpomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo.
Wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate wakiwamkabidhi Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga mara baada ya kumtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kwaajili ya kushaherekea pamoja na kujitathimini katika wiki ya huduma kwa wateja ambapo benki hiyo imeadhimisha mwaka huu kwa kuwatembelea wateja wake mahali walipo.


Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga mwenye miwaniakizungumza na wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo  ikiwa ni adhima ya benki hiyo kuwatembelea wateja wake.
Mfanyakazi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) akizungumza na wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo  mara baada ya kuwatembelea ofisini kwao.
















Picha za pamoja za wafanyakazi  wa benki ya TIB Corporate.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad