HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 11, 2018

WAMBURA AWAONYA WAAMUZI, LIGI KUENDELEA WIKIENDI HII

 Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi  Boniface 

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
LIGI kuu Tanzania Bara inatarajia kuendelea tena mapema wikiendi hii kwa timu zote 20 kuanza kukamilisha  mzunguko wa nne  wa ligi huku timu za Simba, Yanga na Azam ratiba zao za zikitafutiwa ratiba nyingine.

Akizungumzia ratiba ya ligi, Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi  Boniface Wambura amesema mzunguko wa nne wa ligi utaanza wikiendi hii baada ya kumalizika kwa ratiba ya michezo ya kimataifa ya kirafiki ya FIFA iliyochezwa tarehe 3 hadi 11 Septembe.

Amesema kutokana na kalenda ya FIFA, kuna baadhi ya mechi za Simba, Yanga na Azam zuki zilizoondolewa kwa ajili ya kupisha ratiba hiyo na wao kuwa na mechi pungufu baada ya  wachezaji wao kwenda katika timu za taifa na kupelekea kuhairisha mechi zao.

Wambura amesema kuwa, kwa timu zilizokuwa hazijakilimisha mzunguko wa pili na wa tatu watapangiwa tarehe ya kucheza mechi zao kwani kwa sasa kutakuwa na ligi ndefu ,mechi nyingi 380 na hiyo ni  kutokana na timu kuwa nyingi.

"timu ambazo hazijafanikiwa kufikisha idadi ya mzunguko wa mechi zao na watapangiwa ratiba ili kucheza mechi hizo, ila kwa sasa ligi itakuwa ndefu na itahitaji umakini mkubwa kutokana na timu kuwa nyigi,"amesema Wambura.

Akizungumzia kuhusu waamuzi wa ligi kuu kutokuwa makini katika maamuzi yao uwanjani, Wambura amesema kuwa waamuzi waliofanya makosa katia mzunguko wa kwanz ana wa pili tayari wameshawachukulia hatua na kuwataka waamuzi wengine kuchezesha mpira wa kutumia kanuni 17 za mpira.

Wambura amesema, waamuzi wanatakiwa waangalie mechi zao zilizopita pamoja na kufanya mazoezi kwa sana na hii inatokana na idadi ya mechi 
na msimu huu watakuwa wamepata mechi nyingi za kuchezesha.

Amesisitiza kwa sasa wana waamuzi makini wakiwa wanasimamiwa vizuri na kamati ya waamuzi na hawatasita kwuachukulia hatua wale ambao watashindwa kuchezesha kwa sheria 17 za soka.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad