HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 6, 2018

Wafanyabiashara wahimiza kuwekeza India

Mwenyekiti mstaafu wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Ltd, Dk Reginald Mengi akibadilishana mawazo na Balozi wa India nchini Mh. Sandeep Arya mara baada ya kuwasili kwenye mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti mstaafu wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Ltd, Dk Reginald Mengi akisalimiana na Kaimu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo – TCCIA Bw.Octavian Mshiu (aliyeipa kisogo kamera) wakati wa mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya ONGC Petro additions Limited ya nchini India, Avinash Joshi.
Katibu Mkuu (idara ya usambazaji maji) na Mwenyekiti wa GWSSB wa Serikali ya Gujarat nchini India, J.P. Gupta akieleza fursa zilizopo katika maeneo mbalimbali jimbo la Gujarat nchini India wakati wa mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti mstaafu wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Ltd, Dk Reginald Mengi akizungumza na wafanyabiashara wa jimbo la Gujarat na Tanzania wakati wa mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Shirikisho la wenye viwanda nchini CTI Bw. Shubhash Patel akizungumza na wageni waalikwa wakati wa mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya ONGC Petro additions Limited ya nchini India, Avinash Joshi, Mwenyekiti mstaafu wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Ltd, Dk Reginald Mengi, Balozi wa India nchini Mh. Sandeep Arya pamoja na Katibu Mkuu (idara ya usambazaji maji) na Mwenyekiti wa GWSSB wa Serikali ya Gujarat nchini India, J.P. Gupta wakifurahi jambo wakati wa risala ya Mwenyekiti wa Shirikisho la wenye viwanda nchini CTI Bw. Shubhash Patel (hayupo pichani) katika mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) Bw.Octavian Mshiu akihitimisha wakati wa semina maalum kwa wafanyabiashara wa Tanzania walipokutana na wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat iliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.




Pichani juu na chini ni sehemu ya Wafanyabishara kutoka Tanzania walioshiriki mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti mstaafu wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Ltd, Dk Reginald Mengi akisalamiana Mtalaam Mshauri wa Mambo ya Biashara, Bw. Victor Tesha (kulia) wakati wa mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa India nchini, Bw. Gagan Gupta.
Mwenyekiti mstaafu wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Ltd, Dk Reginald Mengi akibadilishana ‘contact’ na wafanyabiashara wa jimbo la Gujarat mara baada ya kumalizika kwa mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa India nchini, Bw. Gagan Gupta.
Mwenyekiti mstaafu wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Ltd, Dk Reginald Mengi akipiga picha za ukumbusho na baadhi ya wafanyabiashara wa Tanzania katika sekta mbalimbali waliohudhuria mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Sektretarieti iliyoandaa mkutano huo kutoka jimbo la Gujarat katika picha ya pamoja na meza kuu mara baada ya kumalizika kwa mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat 2019 uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.

Meza kuu katika picha Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya ONGC Petro additions Limited ya nchini India, Avinash Joshi, Mwenyekiti mstaafu wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Ltd, Dk Reginald Mengi, Balozi wa India nchini Mh. Sandeep Arya pamoja na Katibu Mkuu (idara ya usambazaji maji) na Mwenyekiti wa GWSSB wa Serikali ya Gujarat nchini India, J.P. Gupta, Mwenyekiti wa Shirikisho la wenye viwanda nchini CTI Bw. Shubhash Patel, Kaimu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) Bw.Octavian Mshiu pamoja na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa India nchini, Bw. Gagan Gupta.


Wafanyabiashara wa Tanzania wamehamasishwa kushiriki maonyesho ya Kimataifa ya Biashara katika Jimbo la Gujarat nchini India ili kupata fursa ya kufanya biashara na uwekezaji.
Hayo yamezungumzwa katika mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka jimbo hilo waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat 2019.
Jimbo la Gujarat lina pato la ndani la dola za Marekani bilioni 15 na linachangia asilimia 17 ya pato la viwanda nchini India na ni jimbo lenye viwanda vikubwa duniani.
Jimbo hilo pia linatoa mchango wa mauzo ya nje kwa asilimia 22 na asilimia 40 ya mizigo inayosafirishwa nchini india.
Akielezea Fursa za Uwekezaji zilizopo Gujarat katika semina maalum kwa wafanyabiashara wa Tanzania jijini Dar es salaam, Balozi wa India nchini Bw. Sandeep Arya amesema Watanzania wana fursa kubwa ya kushiriki uchumi wa Gujarat kwa kuona maeneo ya kushrikiana kiuchumi katika pande hizo mbili.
Akizungumza katika  mkutano huo Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk Reginald Mengi, ambaye ni   Mwenyekiti mstaafu wa TPSF, aliwataka wawekezaji wa India kuja nchini kuwekeza kwa ubia na Watanzania, hususan katika maeneo ya utafiti,  ubunifu na  uongezaji thamani kwa mazao ya kilimo.
Aidha Mwenyekiti wa Shirikisho la wenye viwanda nchini CTI Bw. Shubhash Patel, Kaimu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo – TCCIA Bw.Octovian Mshiu walisema mkutano huo ni muhimu katika kuendeleza ushirikiano wa kibiashara baina ya Tanzania na India wenye historia ndefu.
Naye Katibu Mtendaji wa Chama cha watengeneza vitambaa vya nguo na  mavazi (TEGAMAT), Adam Zuku amesema kuwa semina hiyo  ina maana kubwa kwa watanzania  hasa viwanda vya nguo.
Alisema Tanzania inahitaji kufufua viwanda vyake vya nguo ili viweze kutoa ajira na pia kuwa na matumizi ya pamba yetu.
Alisema kuna changamoto kubwa katika viwanda vya nguo nchini, tatizo la soko linalotokana na nguo zinazotoka nje zinazosababisha tatizo kwenye ushindani sokoni.
Alisema nguo zinazozalishwa nchini zinakuwa ghali kulingana na zinazotoka nje na hivyo kuyumbuisha viwanda vya nguo nchini.
Alisema teknolojia si tatizo, tatizo ni wananchi kuwa wazalendo na kununua bidhaa zao ili kuwezesha viwanda kuendelea kuwapo.
Katika mkutano huo alisema wakati umefika kwa Wafanyabiashara na wadau mbalimbali nchini kushiriki katika fursa za uwekezaji kwenye nguo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad