HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 25, 2018

WAFAMASIA NCHINI WAASWA KUTOA HUDUMA BORA YA BIDHAA ZA DAWA

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
Utaratibu wa kubadilishana dawa kwa mgonjwa mmoja kwenda kwa mtu anayejisikia kuumwa hawaufai kwa afya badala yake anayejisikia kuumwa kupima.

Hayo ameyasema Rais wa Chama cha Wafamasia Tanzania (PST) Issa Hango wakati wa maadhimisho ya siku Wafamasia Duniani ambayo hufanyika Septemba 25 ya Mwaka.

Amesema kuwa katika kuadhimisha siku hiyo ni wito kwa Wafamasia kufanya kwa weledi katika kuangalia afya za wananchi katika kutoa elimu ya matumizi sahihi ya dawa.

Hango amesema kuwa kuna kuwa dawa za maji zikishafunguliwa zinatakiwa kukaa kwa muda wa mwezi mmoja.

Aidha Hango amesema kuwa uweledi mwingine ni pamoja kutoa ushauri dawa zingine zisitumike katika matumizi ya dawa za kulevya.
Amesema  maadhimisho hayo ni pamoja na kufanya tathmini kwa Wafamasia kilichopatikana katika utoaji wa huduma katika jamii.
"Hatuwezi kuacha jamii yetu iangamie katika matumizi ya dawa wakati tunauwezo wa kutoa huduma hiyo kutokana taaluma tulionayo"amesema Hango.

Mwakilishi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Grace Shimwela amesema kuwa TFDA itaendelea kufanya tathmini katika katika Udhibiti wa bidhaa ya dawa ikiwa ni kuwalinda watumiaji wa bidhaa hiyo.
Shimwela amesema kuwa wakifanya tathmini hiyo ni pamoja kuangalia    njia sahihi katika uteketezaji bidhaa za dawa ambazo zimebainika kuwa na madhara.

"Tutaendelea kudhibiti bidhaa za dawa kwa uweledi ili kufanya wananchi wapate huduma bora ya bidhaa za dawa"amesema Shimwela.
 Mwakilishi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Grace Shimwela akizungumza katika Siku ya Wafamasia kuhusiana na Mamlaka hiyo kujipanga katika Udhibiti wa bidhaa za dawa.(Picha na Emmanuel Massaka wa Global ya jamii)
 Katibu Mkuu wa Chama cha Wafamasia Tanzania (PST) Geofrey Yambayamba akizungumza kuhusiana na mikakati ya Wafamasia katika kutoa huduma bora ya bidhaa za dawa
 Picha ya pamoja
Rais wa Chama cha Wafamasia Tanzania (PST) Issa Hango akizungumza katika mkutano wa Wafamasia katika Siku ya Wafamasia Duniani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad