HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, September 15, 2018

SERIKALI INATAMBUA NA KUHESHIMU MCHANGO WA ASASI ZA KIRAIA-WAZIRI UMMY MWALIMU

Mkurugenzi wa Watoto toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Margaret Mussai akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii kwaniaba ya waziri wa wizara hiyo. Mkutano huo uliandaliwa na taasisi ya NAMA Foundation kwa kushirikiana na asasi ya An Nahl Trust.
Mwenyekiti wa Asasi ya An Nahl Trust, Mhandisi Alliy Kilima akizungumza kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii nchini Tanzania ulioandaliwa na asasi yake kwa kushirikiana na NAMA Foundation leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki katika Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii nchini Tanzania ulioandaliwa na NAMA Foundation kwa ushirikiano na Asasi ya An Nahl Trust wakiwa katika mkutano huo leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki katika Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii nchini Tanzania ulioandaliwa na NAMA Foundation kwa ushirikiano na Asasi ya An Nahl Trust wakiwa katika mkutano huo leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya washiriki wa Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii nchini Tanzania ulioandaliwa na NAMA Foundation kwa ushirikiano na Asasi ya An Nahl Trust wakiwa katika mkutano huo leo jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa asasi ya An-Nahl Trust, akizungumza katika mkutano huo. 
Sehemu ya washiriki wa Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii nchini Tanzania ulioandaliwa na NAMA Foundation kwa ushirikiano na Asasi ya An Nahl Trust wakiwa katika mkutano huo leo jijini Dar es Salaam. 

SERIKALI inatambua na kuthamini juhudi za wadau mbali mbali zinazofanywa zenye lengo la kuhakikisha maendeleo ya Watanzania yanawezeshwa kikamilifu, hasa zinazochochewa na asasi za kiraia. 

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalim katika hotuba yake iliyosomwa na Mkurugenzi wa Watoto wa wizara hiyo, Margaret Mussai alipokuwa akifungua Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii ulioandaliwa na taasisi ya NAMA Foundation.

Akizungumza katika mkutano huo ulioshirikisha asasi mbalimbali za kiraia, alisema Serikali inafarijika kuona wadau wakiungana na kupanga mikakati ya kufikia malengo ya mafanikio ya utendaji kwa pamoja kuihudumia jamii.

“...Asasi za kiraia mmekuwa muhimili muhimu kwenye kuhimiza maendeleo ya jamii, mmekuwa mnabuni miradi mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha vijana na wanawake kiuchumi na kutoa huduma za maendeleo ya Jamii kwa kutumia gharama nafuu na hata muda mwingine kwa kutumia rasilimali za wanaojitolea,”

“...Tunatambua mchango wa asasi nyingi za kiraia zinazotoa elimu juu ya mapambano ya magonjwa yanayoambukizwa, mila na desturi zenye madhara kwa vijana wakiwemo watoto wa kike na wanawake. Lakini pia kuna asasi zinazowezesha vijana kuwekeza kiuchumi katika miradi midogomidogo ya uzalishaji mali,” alisema Ummy katika hotuba hiyo.

Aidha alisema licha ya Serikali kutambua mchango mkubwa wa asasi za kijamii, alizitaka kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu na ushirikishwaji wa rika zote, huku zikizingatia sheria na katiba ya nchi ili kufikia malengo yao.

Alizipongeza asasi za An Nahl Trust pamoja na NAMA Foundation kwa kufanikisha mkutano huo uliowakutanisha kwa pamoja wadau mbalimbali toka asasi za kiraia kuwajengea uwezo ukiwa na lengo la kuwajengea uwezo katika shughuli wao.

Kwa pande wake Mwenyekiti wa An Nahl Trust, Mhandisi Alliy Kilima alisema mkutano wa mwaka huu umekuja na maudhui mapana zaidi kuliko ule wa mwaka jana na umedhamiria kutoa taarifa kuhusu Maeneo yanayo lengwa na NAMA na Washirika wake ambayo ni 'Kuwezesha sekta ya Elimu, Kuwezesha sekta ya asasi za kiraia na Kuwawezesha vijana,' Na uwezeshaji wenyewe ni ule ule katika kukuza vipaji, maarifa, stadi na jinsi ya kuyaangalia mambo kwaupana wake. 

Alisema mkutano huo utakuwa na watoa mada wataalam wa masuala mbalimbali watakao wajengea uwezo washiriki hususan katika mafunzo na idili za kujiendesha kwa kufuata taratibu na misingi mwafaka katika asasi zao.
Baadhi ya washiriki katika Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii nchini Tanzania ulioandaliwa na NAMA Foundation kwa ushirikiano na Asasi ya An Nahl Trust wakiwa katika mkutano huo leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki katika Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii nchini Tanzania ulioandaliwa na NAMA Foundation kwa ushirikiano na Asasi ya An Nahl Trust wakiwa katika mkutano huo leo jijini Dar es Salaam. 
Sehemu ya washiriki wa Mkutano wa Uwezeshaji wa Asasi za Kijamii nchini Tanzania ulioandaliwa na NAMA Foundation kwa ushirikiano na Asasi ya An Nahl Trust wakiwa katika mkutano huo leo jijini Dar es Salaam. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad