LUSUNGU HELELA-DODOMA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi ametoa 
rai hiyo leo alipokuwa akiwaaga watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii kufuatia 
kustaafu kwake rasmi Jeshini na kwa mujibu wa sheria kama Katibu Mkuu mnamo 
tarehe 16 Septemba mwaka huu  na kuwataka watumishi hao kufanya kazi kwa weledi 
na nidhamu ya hali ya juu 
 
Meja Jenerali Mstaafu, Milanzi ameelezea kufurahishwa kwake na ushirikiano alioupata 
kutoka kwa watumishi wa Wizara hiyo na kuelezea kuwa, ndio umemwezesha 
kuiongoza vema wizara hiyo kwa kipindi alichokuwepo madarakani na kupelekea 
mafanikio makubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo Wanyamapori, Utalii, Misitu na 
Nyuki na Malikale. 
 
Ameongeza kuwa, Wizara ya Maliasili na Utalii imepata mafanikio makubwa katika  vita 
dhidi ya ujangili  ambayo ni matokeo ya ushirikiano mzuri uliopatikana kutoka kwa 
watumishi wa Wizara, wananchi, Serikali pamoja na wadau mbalimbali wa 
Wanyamapori. 
 
“Katika Kipindi tulichokuwa  pamoja, kuna mambo mengi tumeyakamilisha. Nimefanya 
kazi nanyi na kila mmoja wenu alikuwa akinisaidia ili Wizara yetu iweze kusonga mbele. 
Hakuna hata mmoja aliyeonyesha kutaka kunikwamisha. Ninawashukuru 
sana”Amesema Meja Jenerali Mstaafu,  Milanzi. 
 
Akizungumza kwenye hafla fupi ya kumuaga Meja Jenerali Mstaafu, Gaudence Milanzi 
iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa UDOM jijini Dodoma  na kuhudhuriwa na 
watumishi wapatao 113 wa Wizara hiyo, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. 
Aloyce Nzuki, amempongeza Meja Jenerali Mstaafu, Milanzi kwa kustaafu rasmi jeshini 
na kwa mujibu wa sheria kama Katibu Mkuu wa Wizara hiyo. 
 
Amemsifu Meja Jenerali Mstaafu, Milanzi kwa umahiri wake katika utendaji hasa namna 
alivyoweza kufanya kazi na raia kwa ushirikiano wa hali ya juu wakati yeye ni 
Mwanajeshi. 
 
“ Umefanya mambo makubwa kwa kuweka mifumo mizuri pamoja na kubuni mikakati 
na mbinu za kutatua changamoto zilizokuwa zinaikabili Wizara kiutendaji na 
kuhakikisha watumishi wanapata utulivu wa akili kwa kujali maslahi ya watumishi na 
haki zao na hivyo kuwawezesha kufanya kazi wakiwa na utulivu wa akili jambo 
liliongeza ufanisi katika kazi.”ameelezea Dkt. Nzuki. 
 
Akitoa Shukrani kwa ushirikiano alioupata kutoka kwa Dkt. Nzuki wakati akiiongoza 
Wizara hiyo, Meja Jenerali Mstaafu, Gaudence Milanzi amesema, amepata ushirikiano 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi ( kulia) akizungumza na watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii wakati akiwaaga leo jijini Dodoma kufuatia kustaafu kwake rasmi Jeshini na kwa mujibu wa sheria kama Katibu Mkuu mnamo tarehe 16 Septemba mwaka huu ambapo amewataka watumishi hao kufanya kazi kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Aloyce Nzuki.
 Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Maliasili wakiwa wamesimama kwa muda wa dakika moja mara ikiwa ni ishara ya kuwakumbuka wale wote waliopoteza maisha kufuatia ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV. Nyerere.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi ( katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Menejimenti ya Wizara kabla ya kuzungumza na Watumishi wa Wizara hiyo kwa ajili ya kuwaaga leo jijini Dodoma kufuatia kustaafu kwake rasmi Jeshini na kwa mujibu wa sheria kama Katibu Mkuu mnamo tarehe 16 Septemba mwaka huu. .
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi ( kushoto) akizungumza na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Aloyce Nzuki (kulia) mara baada kumaliza kuwaaga Watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii leo jijini Dodoma kufuatia kustaafu kwake rasmi Jeshini na kwa mujibu wa sheria kama Katibu Mkuu mnamo tarehe 16 Septemba mwaka huu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi ( wa pili 
kushoto) akizungumza na  Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Aloyce Nzuki (wa 
kwanza kushoto) akiwasili kwa ajili ya  kuwaaga  Watumishi wa Wizara ya Maliasili na 
Utalii  leo  jijini Dodoma  kufuatia kustaafu kwake rasmi Jeshini na kwa mujibu wa 
sheria kama Katibu Mkuu mnamo tarehe 16 Septemba mwaka huu ambapo 
amewataka watumishi hao kufanya kazi kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu. Wengine 
ni Wasaidizi wake.
(PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA-MNRT) 




No comments:
Post a Comment