HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 27, 2018

VIWANDA VYA SARUJI VYATAKIWA KUZALISHA SARUJI YA KUTOSHA PAMOJA NA KUSIMAMIA BEI YA SOKONI

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
SERIKALI imesema kuwa wenye viwanda vya saruji wazalishe saruji ya kutosheleza mahitaji ya ndani pamoja na kusimamia bei ya bidhaa hiyo mpaka kwa mlaji wa mwisho.

Hayo ameyasema Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charle’s Mwijage wakati alipotembelea viwanda vya Saruji vya Camel na Twiga , amesema amekosa hivi usingizi kwa kuadimika kwa saruji nchini na kuwataka viwanda hivyo vizalishe saruji ya kukidhi mahitaji ya ndani kutokana na kuwepo miradi mbalimbali ya ujenzi.

Mwijage amesema kuwa hivi karibuni kulikuwa kuadimika kwa saruji iliyotokana na baadhi ya viwanda kuwa katika matengenezo pamoja na makaa ya mawe kuzalishwa kwa kiwango kidogo.

Amesema kuwa katika kusimamia wizara hiyo kwa mzalishaji ambaye hatakwenda na kasi ya uzalishaji wa saruji anatomlaka ya kuifuta leseni hivyo wenye viwanda lazima wakidhi mahitaji ya saruji.

Aidha amesema kuwa kwa mwaka tani milioni 10.5 zinalishwa hivyo lazima kila kiwanda kiongeze uzalishaji na kuweza kuuza hata masoko ya nje ya nchi kwa kupata fedha za kigeni zinazotokana na saruji.


Amesema kuwa kuna viwanda vitatu vya saruji vinajengwa nchini ambavyo vitaongeza uzalishaji wa wa saruji hiyo.

Mwijage amesema kuwa viwanda vikizasha saruji na kuweza kuuza katika masoko ya nje kuna uwezekano wa bidhaa ya saruji ikwa inachangia uchumi wa nchi na kuongoza katika uchangiaji huo kwa pato la taifa.

Meneja wa Masoko wa kiwanda cha Saruji cha Twiga , Danford Semwenda amesema kuwa kwa sasa wanazalisha tani 6000 kutoka tani 300O kwa siku 15 zilizopita iliyotokana na matengenezo ya mtambo.
Waziri Mwijage leo Augusti 27,2018 ametembelea viwanda vya kutengeneza Saruji kuanzia cha Camel kilichopo Mbagala rangi Tatu na cha Twiga kilichopo Tegeta jijini Dar es Salaam.




 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akizungumza na viongozi wa kiwanda cha saruji cha Camel kilichopo Mbagala rangi tatu jijini Dar es Salaam.
 Mkurugezi Mtendaji wa Kiwanda cha Camel akitoa baadhi ya taarifa kwa 
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage kuhusiana na uzalishaji wa kiwanda hicho na jinsi wanavyokidhi soko jijini Dar es Salaam.

 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akitembelea kiwanda cha Camel kilichopo Mbagala jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuangalia utendaji kazi wa kiwanda hicho kutokana na kukosekana kwa saruji hapa nchini.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akipewa maelezo na Mkurugenzi mtendajiwa kiwanda cha kuzalisha Saruji cha Camel, Gharibu Hamis jijini Dar es Salaam leo Augusti 27,2018 mara baada ya waziri huyo kutembelea kiwanda hicho.

 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akioneshwa baadhi ya maeneo ya kiwanda cha Camel kilichopo Mbagala jijini Dar es Salaam.

  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akitembelea kiwanda cha kutengeneza Saruji cha Camel kilichopo Mbagala jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akipewa maelezo ya mchanga wa kutengenezea saruji katika kiwanda cha kutengeneza Saruji cha Camel jijini Dar es Salaam leo na Mkurugezi Mtendaji, Gharibu Salum wa Kiwanda cha Camel kilichopo Mbagala jijini Dar es Salaam leo, Augusti27,2018.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda cha Twiga,Alphonso Velez leo Augusti 27,2018 mara baada ya waziri huyo kutembelea kiwanda hicho.



  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akitembelea kiwanda cha Twiga kilichopo Tegeta jijini Dar es Salaam na kushoto ni Mkurugenzi Mkuuwa Kiwanda cha Twiga, Alphonso Velez


  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akionyesha baadhi ya mtambo wa Kiwanda cha Twiga Tegeta jijini Dar es Salam na kupata maelezo ya mtambo huo kutoka kwa Mkurugezi Mkuu wa kiwanda cha Twiga Tegeta,Alphonso Velez.



 Baadhi ya mitambo ya kiwanda cha Twiga Tegeta jijini Dar es Salaam.
 Mchanga wa kutengeneza Saruji katika kiwanda cha Saruji cha Twiga Tegeta jijini Dar es Salaam.
  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akizungumza jijini Dar es Salaam leo alipotembelea kiwanda cha Twiga Tegeta jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Masoko wa kiwanda cha Saruji cha Twiga , Danford Semwenda akijibu swali kutoka kwa  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alipotembelea kiwanda cha Twiga kilichopo Tegeta jijini Dar es Salaam.Kulia ni Mkurugenzi Mkuuwa kiwanda cha Twiga kilichopo Tegeta jijini Dar es Salaa, Alfonso Velez.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad