HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 13, 2018

Rais Magufuli ateua Wakurugenzi wapya Leo

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi akitangaza majina ya, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji walioteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 13/08/18. PICHA NA IKULU

RAIS John Magufuli leo tarehe 13 Agosti, 2018 amefanya mabadiliko madogo ya wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri mbalimbali nchini.

Uteuzi huo alioufanya Rais Magufuli umetangazwa leo Ikulu jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi.

Mabadiliko hayo ni pamoja na, uhamisho wa Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Msafiri Simion aliyehamishiwa wilayani Chato, wakati Senyi Ngaga akipelekwa Kwimba. Hapo chini kuna Orodha ya Wakurugenzi.
 
Mkoa wa Arusha:
Jiji la Arusha: Mkurugenzi ni Maulid Suleiman Madeni( Mpya)

Halmashauri ya Meru: Mkurugenzi ni Emanuel Mkongo( Mpya)

Mkoa wa Dar es Salaam
Manispaa ya Temeke: Mkurugenzi ni Rusubilo Mwakabibi aliyetoka Wilaya ya Kakonko

Ubungo: Mkurugenzi ni Beatrice Kwayi aliyetokea Mtwara

Ilala: Mkurugenzi ni Jumanne Kyango Shauri aliyetoka Korogwe

Kigamboni: Mkurugenzi ni Mwilabusu Ndatwa Rudigija aliyetoka Wilaya ya Rudewa

Mkoa wa Dodoma
Kondoa: Mkurugenzi ni Msitafa Ysyf( Mpya)

Kondoa mji: Mkurugenzi ni Msoreni Juma Dakawa( Mpya)

Mpwapwa: Mkueugenzi ni Paul Mamba Swea( Mpya)

Kongwa: Mkurugenzi ni Dkt, Omary Nkuru( Mpya)

Mkoa wa Geita
Nyankwale: Mkurugenzi ni Maria Caaurembo(Mpya)

Chato: Mkurugenzi ni Eliud Reonard aliyetoka Misungwi

Mkoa wa Iringa
Iringa Manispaa: Mkurugenzi ni Ahamed Njomvu aliyetoka Manispaa ya Sumbawanga

Mkoa wa Kagera
Halmashauri ya Misenyi: Mkurugenzi ni Innocent Mkandala(Mpya)

Bukoba Manispaa: Mkurugenzi ni Benard Moris aliyetoka Misenyi

Halmashauri Bukoba: Mkurugenzi ni Solumon Kimilike(Mpya)

Mkoa wa Katavi
Halmashauri ya Simbo: Mkurugenzi ni Ramadhan Mohamed(Mpya)

Mkoa wa Kigoma
Kigoma: Mkurugenzi ni Smith Pangani ametoka Halmashauri Simbo

Kakonko: Mkurugenzi ni Masumbuko Magangira(Mpya)

Halmashauri Kigoma: Mkurugenzi ni Upendo Erick Mangali(mpya)

Mkoa wa Kilimanjaro
Mwanga: Mkurugenzi ni Kimoro Lubuva

Moshi: Mkurugenzi ni Tatu Selemani Kikwete katokea Halmashauri ya Kibaha

Mkoa wa Lindi
Halmashauri Liwale: Mkurugenzi ni Bakari Mbaga aliyetokea Temeke

Kilwa: Mkurugenzi ni Renatus Mchau(Mpya)

Mkoa wa Mara
Msoma: Mkurugenzi wake ni Kayombo John ametoka Ubungo

Butiama: Mkurugenzi wake ni Mgarani Alfonce(Mpya)

Mkoa wa Mbeya
Mbeya: Mkurugenzi wake ni Edward Katemba ametoka Kigamboni.

Jiji Mbeya: James Kasusula( mpya)

Kyela: Mkurugenzi wake ni Lucy Mganga( Mpya)

Mkoa wa Morogoro
Halmashauri ya Kilombelo: Mkurugenzi wa ni Eng. Stephan Kaliwa(Mpya)

Halmashauri ya Morogoro: Mkurugenzi ni Kayombe Ryoba(Mpya)

Malinyi: Mkurugenzi ni Mussa Elias Mnyeti

Kilosa :Mkurugenzi ni Lucas Mwambambale(Mpya)

Mkoa wa Mtwara
Mtwara: Mkurugenz ni Kanali Emanuel Mwaigobeko

Mkoa wa Mwanza
Misungwi: Mkurugenzi ni Kisena Magena(Mpya)

Ukerewe :Mkurugenzi ni Esther Chaura(Mpya)

Mkoa wa Njombe
Waging'ombe :Mkurugenzi ni Philip Lukoa ametoka Chalinze

Ludewa ;Mkurugenzi ni SUnday George(Mpya)

Mkoa wa Pwani
Chalinze: Mkurugenzi ni Amina Mohamed Kiwanuka aliyetoka Waging'ombe

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad