HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, August 28, 2018

CAF YARIDHISHWA NA MAANDILIZI YA AFCON

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (C)akipokea Bendera ya CAF kutoka kwa Rais wa  Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) Ahmad Ahmad baada ya mazungumzo ya kikazi katika Ofisi ndogo ya Waziri Mkuu Jijini Dar es Salaam Agosti 27/2018.kushoto kwa Waziri Mkuu ni Waziri wa Michezo na Utamaduni Dkt Harisson Mwakembe.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja Rais wa Shirikisho la Soka Barani Aafrika  (CAF ). Ahmad Ahmad, Waziri Mkuu ni Waziri wa Michezo na Utamaduni Dkt Harisson Mwakembe pamoja na viongozi wa mpira wa Tanzania.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiagana na Rais wa Shirikisho la Soka Barani Aafrika  (CAF ). Ahmad Ahmad . baada ya mazungumzo ya kikazi  katika ofisi ndogo ya Waziri Mkuu Jijini Dar es Salaam  Agosti 27/2018

RAIS wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Bw. Ahamd Ahmadamesema ameridhishwa na maandalizi ya michuano ya Afrika ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (AFCON).

Mashindano ya mpira wa miguu kwa Vijana wenye umri wa chini ya  miaka 17 AFCON yanayotarajiwa kufanyika mwaka 2019 nchini Tanzania.

Ameyasema hayo Jumatatu, Agosti 27, 2018 wakati akizungumza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Pia ameihakikishia Serikali kwamba hakuna mabadiliyo yoyote ya ratiba yatakayofanyika kuhusu wenyeji wa mashindano na kwamba CAF itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kufanikisha michuano hiyo.

Rais wa CAF yupo nchini kwa ajili ya kuongoza mkutano maalum wa mabadiliko ya katiba ya Baraza la Vyama vya Soka katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).

Mkutano huo unaofanyika jijini Dar es Salaam, umehudhuriwa na viongozi wa juu wa nchi wanachama wote 12 wa CECAFA wakiwemo marais.

Kwa upande wake,Waziri Mkuu WAZIRI amesema mechi zoteza michuano ya Afrika ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (AFCON) zitafanyika jijini Dar es Salaam.mashindano

“Tupo katika hatua za mwisho za maandalijzi ya michuano hiyo itakayofanyika jijini Dar Es Salaam katika viwanja vya Taifa, Uhuru, Chamanzi na JK Park utatumika kwa mazoezi.”

Waziri Mkuu amesema ni muhimu kwa nchi kushiriki katika mashindano makubwa kama hayo kwa kuwa yanasaidia kwenye ukuzaji wa vipaji kwa vijana ambao wengi wao ni wanafunzi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad