HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, July 23, 2018

Wafanyakazi wa JKCI wamuaga Afisa Muuguzi Mwandamizi Mama Hadija Mradi aliyestaafu utumishi wa Umma

 Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mama  Hadija Mradi (kulia) akikata keki wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa  Taasisi hiyo ilizopo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uuguzi  Robert Mallya
 Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uuguzi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akimlisha keki Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu Mama  Hadija Mradi wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo katika  ukumbi wa mikutano wa  Taasisi hiyo uliopo jijini Dar es Salaam . Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Prof. Mohamed Janabi (kushoto) akimkabidhi cheti cha kutambua mchango wake katika utumishi wa umma kwa kufanya kazi kwa miaka 41 Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu Mama  Hadija Mradi katika  hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uuguzi Robert Mallya.
 Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mama  Hadija Mradi (kulia) akifuatilia yaliyokua yakiendelea wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo Delila Kimambo.
Baadhi ya wafanyakazi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokua yakiendelea wakati wa hafla fupi ya kumuaga Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu Hadija Mradi (hayupo pichani) iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo uliopo jijini Dar es Salaam. Picha na JKCI

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad