HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, July 16, 2018

MADAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA MOYO WA TAASISI YA JKCI WATOA HUDUMA ZA MATIBABU MAONYESHO YA SABASABA

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Delila Kimambo akitoa huduma ya ushauri kuhusu namna ya kuepukana na magonjwa ya moyo wakati wa maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara yaliyofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo katika Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Katika Banda la Taasisi hiyo huduma za matibabu ya moyo zilitolewa bila malipo yoyote zikiwemo dawa kwa wagonjwa wanaokutwa na matatizo.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha ubora wa huduma Tulizo Shem wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akitoa elimu kwa wananchi kuhusu magonjwa ya moyo wakati wa maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara yaliyomalizika hivi karibuni katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo katika Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Katika maonyesho hayo Taasisi hiyo ilishika nafasi ya tatu katika utoaji wa huduma kwa wananchi, huduma za matibabu ya moyo zilitolewa bila malipo yoyote zikiwemo dawa kwa wagonjwa wanaokutwa na matatizo.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo akimwelekeza mtoto kujibu maswali kuhusu afya bora ya moyo wakati wa Maonyesho ya Kimataifa ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yaliyomalizika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Wananchi waliotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakipata huduma ya matibabu ya moyo wakati wa maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara yaliyomalizika hivi karibuni katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo katika Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Katika maonyesho hayo Taasisi hiyo ilishika nafasi ya tatu katika utoaji wa huduma kwa wananchi kwa kutoa huduma bila malipo yoyote zikiwemo dawa na rufaa ya moja kwa moja kwa wagonjwa wanaokutwa na matatizo. Picha na JKCI

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad